• Tidak ada hasil yang ditemukan

Tunapendekeza utafiti ufanywe katika kuchunguza kama kuibuka kwa mashairi ya kisasa yalichangiwa na siasa ama maendeleo ya taaluma katika ngazi ya Chuo Kikuu ama la!

Tunapendekeza pia utafiti ufanyike kuhusu kuchunguza mabadiliko yanayotokea katika mashairi ya kimapokeo ili kuweza kuona kama yanasaidia kuupeleka mbele ushairi wa kimapokeo au hakuna maendeleo yoyote.

MAREJELEO

Abeid, A., (1954). Sheria za Kutunga Mashairi na Diwani ya Amri. Nairobi: EALB. Babbie, E., (1999). The Basics of Social Research. Belmont: Wadsworth Publishing

Company.

Bathes, R., (1994). The Semiotic Challenge. Berkely: University of Califonia Press. Chandler, D., (1992). Semiotics: The Basics, London: Routledge Press.

Chuwa, M., (2011). “Uchunguzi wa Vipengele vya Fani Katika Mashairi ya Mathias Mnyampala”. Tasinifu ya Umahiri, Chuo Kikuu cha Dodoma.

Cohen, L. na Wenzke (2000). Research Methods in Education (5th end) London: Rouledge Press.

Creswell, J.W., (2009). Research Design: Qualitative, Quantitatie, and Mixed

Methods Approaches. Los Angeles: SAGE Publication.

Frolova, N., (2003). “Euphrase Kezilahabi: The Renewal of Kiswahili Poetry”. In

Kiswahili, Vol. 66 Dar es salaam. IKR.

Furlong, P. na Wenzake, (2000). Research Methods and Statistrics: An Integrated

Approach. New York: Harcourt College Publishers.

Haji, G.H., (1994). Kimbunga. Dar es Salaam: TUKI.

John, L., (2004). Critical Reading: A Guide. In http://www. Brocku. Ca/English/jlge/criticalreadig. Html. Accesssed, 30th, October 2006.

Juma, S.R., (2012). “Ufundishaji na Ujifunzaji wa Ushairi wa Kiswahili Katika Shule za Sekondari Jijini Dar es Salaam”. Tasinifu ya Umahiri, Chuo Kikuu cha Dar es Salaam.

Kandoro, S., (1978), Ushahidi wa Mashairi ya Kiswahili na Lugha Yake. Dar es Salaam: Longman Ltd.

Keys, B. na Wenzake (1989). “Four Faces of Fully Function Middle Manger;

California Management Review; Vol. XXIV. No, 4 pp. 59-67.

Kezilahabi, E., (1974). Kichomi, Nairobi: Heinemann Educational books.

Kezilahabi, E., (1977). “Mashari ya Saadan”, Mulika, Namba 14. Dr es Salaam: TUKI. Kur. 32-40.

Kezilahabi, E., (1983). “Uchambuzi katika ushari wa Kiswahili”. Katika Makala ya

Semina ya Kimataifa ya Waandsihi wa Kiswahili, Kur. 145-165. Dar es

Salaam: TUKI.

Kezilahabi, E., (1988). Karibu Ndani Dar es Salam: DUP. Kezilahabi, E., (2008). Dhifa, Nairobi: Vide-Muwa.

Kothari, C.R., (1992). Reserch Methodology: Methods and Techniques. New Delhi: Wiley Eastern Limited.

Kothari, C.R., (2008). Research Methodology: Methods and Techniques. New Delhi: New Age International Publishing Ltd.

Massamba, D.P.B., (1983), “Suala la Ushairi wa Kiswahili”. Katika Makala ya Semina ya Kimataifa ya Waandishi wa Kiswahili-Fasihi namba 3. Dar es Salaam: TUKI.

Mayoka, J., (1984). Mgogoro wa Ushairi na Diwani ya Mayoka. Nairobi: EALB. Mlacha, A.K.S. na Madumulla, J.S., (1991). Riwaya ya Kiswahili. Dar es Salaam:

DUP.

Msokile, M., (1992). Uhakiki: Karibu Ndani. Dar es Salaam: DUP.

Mulokozi, M.M., (1975). “Revolution and Reaction in Swahili Poetry”. In Kiswahili,

Vol. 45/2. Dar es Salaam: IKR, Kur. 46-65.

Mulokozi, M.M., (1996). Fasihi ya Kiswahili. Dar es Salaam: Chuo Kikuu Huria cha Tanzania.

Mulokozi, M.M. na K.K. Kahigi, (1979). Kunga za Ushari na Diwani Yetu, Dar es Salaam: TPH.

Mulokozi, M.M. na T.S.Y. Sengo (1995). History of Kiswahili Poetry [AD 1000-2000]. Dar es Salaam: TUKI.

Newman, W.L., (2006). Social Reserch. Sixth Edition, Boston: Pearson.

Njogu, K. na Rocha, C., (1999). Ufundishaji wa Fasihi: Nadharia na Mbinu. Nairobi, JKF.

Nyangwine, N. na Masebo, J., (2002). Uhakiki Katika Fasihi. Dar es Salaam: Nyambari Nyangwine Publishers

Omary, M., (2011), “Siasa katika Ushairi wa Kezilahabi: Uchunguzi wa Karibu

Ndani (1988) na Dhifa (2008), Tanisifu ya M.A Kiswahili Chuo Kikuu cha

Dar es Salaam.

Robson, C., (2007). How to do a Reserch Project: A guide for under graduate

students, Carton Victoria: Blackwell Publishing.

Said, K., (2010). “Matumizi ya Lugha Katika Nyimbo za Harusi za Kabila la Wazigua. Utafiti mdogo wa Kukamilisha Masharti ya Shahada ya Awali”, Chuo Kikuu Huria cha Tanzania.

Seleman, K. na Mtimbo, A., (2004), “Uhakiki wa Diwani ya Kimbunga”. Utafiti Mdogo wa Kukamilisha Masharti ya Shahada ya Kwanza, Chuo Kikuu Huria cha Tanzania.

Sengo, T.S.Y., (1994). “Utangulizi Katika Kimbunga”. Dar es Salaam: TUKI Senkoro, F.E.M.K., (2011). Fasihi. Dar es Salaam: KAUTTU.

Topan, F., (1974). “Utangulizi katika Kichomi”, Nairobi: Heiremann.

Wamitila, K.W., (2002). Uhakiki wa Fasihi: Misingi na Vipengele Vyake, Nairobi: Phoenix Publishers Ltd.

Wamitila, K.W., (2008). Kanzi ya Fasihi: Misingi ya Uchanganuzi wa Fasihi, Nairobi: Vide-Muwa.

Yin, R.K., (1994). Case Study Research: Design ad Methods, (2nd eds. Thousands Oaks Calif: SAGE publishers.

Waliorejelewa Kupitia Mazungumzo

Mulokozi, M.M., (2009). Mazungumzo Katika Mihadhara ya Umahiri Katika Fasihi, Chuo Kikuu cha Dar es Salaam.

Mulokozi, M.M., (2011), Mazungumzo Katika Mihadhara ya Umahiri Katika Fasihi, Chuo Kikuu cha Dar es Salaam.

Sengo, T.S.Y., (2012), Mazungumzo Katika Semina za Umahiri, Chuo Kikuu Huria cha Tanzania.

Senkoro, F.E.M.K., (2010), Mazungumzo Katika Mihadhara ya Umahiri, Chuo Kikuu cha Dar es Salaam.

VIAMBATISHI

Kiambatishi Namba 1: Mashairi ya Haji Gora Haji yaliyotumika

Uchumi ukwamuliwe, ukwamuke kwa haraka Ukwamuke hima uwe, ukae tunakotaka

Kabisa huko usiwe, kunako janga kutoka Isiwe kuwekaweka, ukwamuliwe uchumi

Tumefanya sote kazi, pori hilo kulifyeka Na kuchimbua ardhi, shamba likakamilika Mbona hamtuulizi, kuvuna kunapofika

Kuzichukuwa nafaka, mkazila peke yenu (Madanganyo,uk. 06).

Tumefanya sote kazi, pori hilo kulifyeka Na kuchimbua ardhi, shamba likakamilika, Mbona hamtuulizi, kuvuna kunapofika

Kuzichukua nafaka, mkazila peke yenu (Madanganyo, uk.06).

Wenye vyao watubana, twaumia masikini La kufanyiza hatuna, hali zetu taabani Kwa sasa kilo ya dona, bei mia ishirini

Wakubwa tuteteeni, wenye vyao watubana (Wenye vyao Watubana, uk.10).

Washindana matajiri, kwa bei siyo utani, Ni pigo kwa mafakiri, tulio hali ya chini

Wezeni kutafakari, wanyonge tu madhilani

Wakubwa tuteteeni, wenye vyao watubana, (Wenye vyao Watubana, uk.10).

Utalii tuukuze, uzidi kuimarika Uimarike uweze, nafasi hiyo kushika Ushike na uingize, madata kuminika Iwe kwa kila dakika, wauinue uchumi

Ukulima ni msingi, kwa dhati tukiushika Utapolima kwa wingi, nafaka bila kuchoka Na matunda kila rangi, yatakayonunulika Kwa madala si shilingi, na kuchangia uchumi

Uvuvi ule wa leo, ambao uliofika Kuendelezwa na huo, pia inahitajika Unao wake upeo, kwa uchumi kunyanyuka

Na juhudi zatakika, kwa kuokoa uchumi (Uokolewe, 05).

Ukimwi vielelezo, vyake vinaendeleza Mtu hasa ni wa mwanzo, yule anajituliza Hupata maambukizo wengine kuwanukiza Hiyo njia, moja wapo, inasambaza Ukimwi.

Damu nayo huchangia, pasi na kuichunguza Yenye vidudu vibaya, mwingine kumwuongeza

Kuona wasaidiya kumbe wamuangamiza

Na hilo ni mojawapo, lisambazalo Ukimwi (Vielezeo, uk.3).

Kimbunga mji wa Siyu, kilichowahi kufika Si kwa yule wala huyu, ilikuwa patashika Kimeing’oa mibuyu, minazi kunusurika Nyoyo zilifadhaika

Nyumba kubwa za ghorofa, siku hiyo zimeruka Zikenenda kwa masafa, kufikia kwa kufika Vibanda vyao malofa, vyote vikasalimika Nyoyo zikafadhaika (Kimbunga, uk.01).

Punda kakosa thamani, sababu vitimbi vyake Milele akawa duni, wala asiheshimike Kwa wake umuhimu, kavunjiwa hadhi yake Ndiyo tabia ya punda, kurusharusha mateke Kuchunga akikushinda, mwachie aende zake.

Punda hakumbuki wema, hata kwa mchunga wake Humpa mwinga mtama, na maji anufaike

Katu haiwi salama, shukurani zake mateke Ndiyo tabia ya punda, kurusha rusha mateke

Paka nakuasa wizi, wacha kuiba samaki, Imekuwa yako kazi, majikoni huondoki Haufai uchokozi, si kizuri kitu hiki

Paka nakuasa wizi, vitoweo usiibe (Paka, uk.22).

Mkia baada kumpa, mambo yakawa mabaya Nguo zake kazitupa, unyani kumrudiya Kaanza kuchupa chupa, mitini akarukiya Akafanana na wenzake, akiwa nyani katimu

Wenzake wakamcheka, wote na kumzomeya Akakosa la kushika, kwa haya kujioneya Majuto yakamfika, akabakia kuliya

Akarudia porini, iliko yake kaumu (Kibwangai).

Kuna hadithi ya kale, kwa babu nimepokeya Kwa manyani zama zile, mkasa ulotokeya Nilikuwa mwanakale, hiyo miaka zingatiya Leo nawadokezeya, kwa nilivyoyafahamu.

Nyani baada kugunduwa, watu wanawaviziya Sababu yake kwa kuwa, hila yao mimea Na ndipo wakaamua, mwenzao kumtumiya

Rushwa kajenga kambi, na kuondoka hataki Afanya kila vitimbi, mkaidi hashikiki Tumzushieni wimbi, isiwe kutuhiliki

Kiambatisho Namba 2: Mashairi ya Kezilahabi yaliyotumika

Nitaandika wimbo juu ya mbawa za inzi Utoe muziki arukapo wa usikie walio wengi Ushairi wa jalalani utaimbwa

Juu ya vidonda vya wakulima Na usaha ulio jasho lao

Nitaandika juu ya mbawa za wadudu wote warukao.

Juu ya mistari ya pundamilia na masikio makubwa ya tembo,

Juu ya kuta vyooni, maofisini, madarasani Juu ya paa za nyumba na kuta za Ikulu! Na juu ya khanga na tisheti

Nitaandika wimbo huu.

Mti mkongwe umelalila upande Wa nyumba zetu hafifu

Upepo mkali uvumapo hatulali Kila kukicha twatazama mizizi yake Na mkao wake, na kuta hafifu za nyumba Lazima ukatwe kuanzia matawi hadi shina Mafuriko ya mwaka huu yaashiria

Tutabaki kuwasimulia wajukuu Mwaka ule wa mafuriko

Miti mingi mikongwe iliaanguka (Mafuriko, uk.4).

Ni chakula cha mchana, Walanchi wameshafika, Wazungu, Wahindi, Waarabu Washateka sehemu zao Chakula ki mezani Nidhifa

Mawaziri wenye kula Wabunge wapewa magari Waandishi waliosajiliwa Watangazaji wenye yale yale Wakereketwa wasokereka Kimya wamekaa (Dhifa, uk. 27).

Na hiki kibanda gani, ghafla mbele yangu Ni kibanda cha Msonge, mlango wake mmoja Mlango wenye uwazi, na ndani moto wawaka, Hodi hodi wenyewe, ni mimi kichwamaji Natafuta zangu njuga, na lile vazi la Kindu

Ingawa sina ubuyu, naja kukesha nanyi (Karibu Ndani, uk.34).

Akiyumbayumba

Na sarawili zee mawinguni

Akitoka magharibu kwenda mashariki Kisha akaanguka baharini kwa kishindo Binadamu tukasubiri. Tukasubiri

Halafu baharini ndege katoka Karuka juu mawinguni Wengine wakasema: Ndiye! Wengine: Siye!

Tukasubiri (Matumaini, uk. 06).

Jibwa likitoka jikoni Ulimi lajilamba Piga limekwiba piga Jibwa likishika hatamu

Haliwezi kuacha utamu, (Jibwa, uk.15).

Azimio sasa ni mabaki ya chakula Kwenye sharubu za bepari

Kalamu inayovuja

Katika mfuko wa mwanafunzi Vumbi zito

Baada ya ng’ombe kupita Kilichosalia sasa

Ni punje za ulezi

Zilizosambazwa jangwani

Sikiliza Monika

Sisi tumezoea vituko vya wakubwa Huyu mumeo anatoka kijiji jirani Tulimwona akilambwa na mbwa Alipomaliza kujisaidia

Na alikimbia siku ya tohara

Sasa naye avuta kidevu shingo upande Kama beberu, tayari kupigana

Wewe Monika

Twende ufukweni kuogelea Tuone hiyo cheni ya dhahabu.

Wewe Monika

Ulitoka kwetu bila ushanga kiunoni Kama kumbikumbi asi mbawa Ulipofika mjini ukaolewa na waziri Sasa wataka tusimame barabarani Kukupungia matawi mabichi Upitapo wainua kipua juu

Chogo limechongoka kama senene Aendaye kwenye harusi ya mende Na kutusanifu kwa mawani meusi Kama nyani achezaye sarakasi

Dokumen terkait