TUME YA KUDHIBITI UKIMWI TANZANIA (TACAIDS)
TAARIFA YA UFUATILIAJI
NA TATHMINI YA UKIMWI
MKOA WA MBEYA
TUME YA KUDHIBITI UKIMWI TANZANIA (TACAIDS)
YALIYOMO
Ukurasa
Orodha ya Vifupisho iv
UtangulizI vii
Shukrani xi
Sura 1:Maoni na Yaliyobainika 1
Sura 2: Changamoto 24 Sura 3: Mafanikio 26 Sura 4: Mapendekezo 32 Hitimisho 33 Vitabu Vilivyorejewa 34 Msamiati wa kiufundi 35
ORODHA YA VIFUPISHO
ACCA Udhibiti wa UKIMWI Katika Makampuni Afrika
AIDS Upungufu wa Kinga Mwilini
ANC Kliniki ya Wajawazito
ART Tiba ya kuongeza Kinga ya Mwili
BACAIDS Tume ya UKIMWI ya BAKWATA
BAKWATA Baraza kuu la Waislamu Tanzania
CARF Mfumo wa Mwitikio wa Jamii Kuhusu Ukimwi
CBO Mashirika ya Kijamii
CHAC Mratibu wa UKIMWI wa Halmashauri ya Wilaya
CHMT Timu ya utawala ya Afya ya Halmashauri ya Wilaya
CMAC Kamati za Kudhibiti UKIMWI katika Mamlaka za Serikali za Mtaa
COPTA Zana ya Mipango Shirikishi ya Jamii Dhidi ya UKIMWI
CPP Mpango wa ushirikiano wa Jamii
CSO Vyama vya Kiraia
DACC Mratibu wa Kudhibiti UKIMWI wa Wilaya
DAS Katibu Tawala wa Wilaya
DC Mkuu wa Wilaya
DED Afisa Mtendaji wa Wilaya
DFID Idara ya Maendeleo ya Kimataifa
DMO Afissa Afya wa Wilaya
DRC Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo
EU Umoja wa Ulaya
FBO Mashirika ya Kidini
GTZ Shirika la Ushirikiano wa Kiufundi wa Ujerumani
HBC Matunzo ya Nyumbani
HIV Virusi vya UKIMWI
HLM Vifaa vya Elimu ya Afya
HSIS Utafiti wa Maambukizo ya Virusi vya UKIMWI/UKIMWI
MARVAD Utafiti wa Dawa za Kuongeza Kinga ya Mwili Mkoani Mbeya
MCC Kampuni ya Simenti ya Mbeya
MCH Afya ya Mama na Mtoto
MMRP Mradi wa Utafiti wa Afya Mbeya
MOHSW Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii
MRACP Mradi wa Kudhibiti UKIMWI Mkoani Mbeya
MSD Duka la Vifaa vya Afya
MTEF Mfumo wa Utekelezaji wa Kati ya Muhula
NACOPHA Baraza Kuu la Taifa la Watu Wanaoishi na Virusi vya UKIMWI
NACP Mpango wa Taifa wa Kudhibiti UKIMWI
NGO Asasi Zisizo za Kiserikali
OVC Watoto Yatima na Wanaoishi Katika Mazingira Magumu
PE Elimu Rika / Mwelimishaji Rika
PEP Hadhari Baada ya Hatari
PLHA Mtu/Watu anayeishi/Wanaoishi na Virusi vya UKIMWI
PLHIV Mtu/Watu anayeishi/wanaoishi na Virusi vya UMIMWI
PLPWHA Mtu/Watu anayeishi/Wanaoishi kwa Matumaini na Virusi vya UKIMWI
PMTCT Uzuiaji wa Uambukizo wa Virusi vya Ukimwi Kutoka kwa Mama
Kwenda Kwa Mtoto
RACC Mratibu wa Kudhibiti UKIMWI wa Mkoa
RAS Katibu Tawala wa Mkoa
RC Mkuu wa Mkoa
REO Afisa Elimu wa Mkoa
RFA Wakala wa Uwezeshaji wa Mkoa
RMO Afisa Afya wa Mkoa
TGPSH Mradi wa Afya wa Tanzania na Ujerumani
TMAP Mpango wa Udhibiti wa UKIMWI Tanzania
TOT Uelimishaji wa Waelimishaji
TRA Mamlaka ya Mapato Tanzania
TV Luninga
UKIMWI Upungufu wa Kinga Mwilini
UN Umoja wa Mataifa
UNAIDS Mpango wa Umoja wa Mataifa wa Kudhibiti UKIMWI
UNV Watu wanaojitolea wa Umoja wa Mataifa
VCR Mtambo wa Kuonyeshea Mikanda ya Video
VCT Ushauri Nasaha na Upimaji wa Hiari wa UKIMWI
VMAC Kamati ya Kudhibiti UKIMWI ya Kijiji
VVU Virusi vya UKIMWI
WMAC Kamati ya Kudhibiti UKIMWI ya Kata
UTANGULIZI
Mkoa wa mbeya una eneo la Kilomita 64,000 za mraba na una jumla ya idadi ya watu 2,070,046. (wanaume 990,825 na wanawake 1,079,221). Jumla ya idadi ya watu waliopo katika rika la kuweza kuzaa (miaka 15 hadi 49) ni 423,945. Kasi ya maambukizi ya UKIMWI ni 13.5%, ni ya pili kwa ukubwa nchini (Kasi ya maambukizi ya UKIMWI ya taifa ni 7%). Mbeya ina mtandao mzuri wa mawasiliano kwani barabara kubwa zinapita mkoani na kuunganisha bandari za Dar es Salaam na Mombasa pamoja na Zambia na Malawi na nchi nyingine za Afrika kupitia barabara na reli na kutengeneza upenyo wenye mchanganyiko wa watu kati ya nchi hizi tatu na zingine za kusini.
Lengo kuu la timu iliyotafiti na kukusanya habari kuhusu hali ya UKIMWI ya mkoa wa Mbeya lilikuwa ni kufanya ufuatiliaji na tathmini ya hali ya UKIMWI ya Mkoa wa Mbeya. Huu ni utaratibu wa kawaida wa mara kwa mara wa TACAIDS wa kutembelea Mkoa ili kupata ufahamu bora zaidi kuhusu afua zinazohusiana na UKIMWI katika Mkoa. Ratiba ilikuwa ni yenye kueleweka sana na ilitengenezwa maalum kwa ajili ya kukutanisha timu na vikundi tofauti vya watu wakiwemo mashirika ya kidini, wasichana na wanaume, wanawake, watu waishio na virusi vya UKIMWI, vikundi maalumu vya walengwa kama wahudumu wa baa na sekta za serikali kama elimu, kilimo na maendeleo ya jamii. Leo UKIMWI unatambulika si tu kama jambo kubwa la kiafya peke yake, bali pia kama tatizo la kijamii na kimaendeleo katika nchi, mkoa, wilaya na jamii kwa ujumla. Ilipokuwa mkoa wa Mbeya timu ilitembelea wilaya nne kati ya wilaya nane zilizopo mkoani humo. Wilaya zilizotembelewa zilichaguliwa na mamlaka za mkoa kwa kushirikiana na mamlaka za wilaya.
TACAIDS walitayarisha orodha ya maswali zilizosambazwa kwa vikundi mbalimbali kabla ya kutembelea vikundi hivyo kwa ajili ya kufanya majadiliano. Timu ya TACAIDS iligawanywa katika timu mbalimbali zilizotembelea vikundi tofauti kama vile wanawake, vijana, watu waishio na virusi vya UKIMWI, (wazee, wahudumu wa baa na wafanyakazi wa nyumba za wageni, mashirika ya kidini, taasisi za elimu, vituo vya
Mbinu iliyotumika ilikuwa shirikishi ambapo vikundi vyote vilihusika katika majadiliano. Lengo la majadiliano lilikuwa ni kufahamisha timu kutoka TACAIDS kuhusu utekelezaji wa shughuli za UKIMWI kimkoa na kupata maoni na ushauri kutoka kwa washiriki wa mjadala kuhusu kuboresha shughuli za kudhibiti UKIMWI katika Mkoa.
Mikutano ya mashauriano ilisaidia TACAIDS kuhamasisha vikundi vya jamii kuelewa kuwa vita dhidi ya UKIMWI ni kwa ajili yao wao wenyewe na si watu wengine. Sababu kama hizi ndizo zinazochochea washika dau katika ngazi za mkoa na wilaya kuendelea kupambana na ugonjwa huu hatari.
Faida za mbinu hii ilikuwa pia ni kutoa msaada katika masuala ya kiufundi kama vile utaratibu wa kuchangisha na utatuzi wa masuala ya pesa ambapo ilitambulika katika majadiliano kuwa kwa baadhi ya wapokea pesa kulikuwa na tatizo hasa katika ufahamu wa utaratibu.
ORODHA YA WASHIRIKI
Taarifa ya UKIMWI ya Mkoa wa Mbeya imetayarishwa na TACAIDS, ambao walituma timu kwenda Mbeya kufanya ufuatiliaji na tathmini wa hali ya UKIMWI katika Mkoa wa Mbeya. Timu ilikuwa na wafanyakazi wa TACAIDS, wawakilishi wa NACOPHA, watumishi wa Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii, mamlaka za afya za kimkoa na kiwilaya, waratibu wa UKIMWI wa Halmashauri za Wilaya, Watumishi wa GTZ (wakala wa uwezeshaji wa mkoa), wabia wa maendeleo kutoka Benki ya Dunia na waandishi wa habari.
TACAIDS
Mh. Lediana Mng’ong’o, Mb, Kamishna Dr. Fatma H. Mrisho, Mwenyekiti Mtendaji Nd. Sam Komba, Mwanasheria
Nd. Charles Kamugisha, Idara ya Mwitikio wa Wilaya na Jamii Nd. Chaddy Anthony, Idara ya Sera na Mipango
Nd. Simon Keraryo, Uraghibishi na Uhamasishaji Mr. Shedrack Mpabangaya, Idara ya Fedha na Utawala Nd. Hulda Tairo-Urasa, Idara ya Fedha na Utawala Baraza la watu wanaoishi na VVU/UKIMWI (NACOPHA) Nd. Vitalis Makayula, Mwenyekiti NACOPHA
Nd.Grace Mwamhonjo, Mjumbe NACOPHA Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii Nd. Joel Ndayongeje, MISO, NACP Mamlaka ya Afya ya Mkoa Mamlaka ya Afya ya Wilaya
Wabia wa Maendeleo
Nd. Angelica Schrettenbrunner, Mratibu wa mradi wa UKIMWI wa GTZ Nd. Yunus Koshuma, GTZ
Dr.Emmanuel Malangalila, Benki ya dunia Waandishi wa Habari
Nd. Benny Mwaipaja, ITV
Nd. Festo Sikagonamo, ITV (kamera) Nd. Niko Mwaibale, TVT
Nd. Ngujuna Kalanja, TVT (kamera) Madereva
Gabriel Chonya Barick Dawa Danstan Kapinga Habib Nzomukonda
SHUKRANI
Tunapenda kutoa Shukrani zetu za dhati kwa wafuatao kwa msaada wao mkubwa katika uandaaji wa taarifa hii: vijana, wanawake, watu waishio na VVU / UKIMWI, wazee, wafanyakazi wa baa, wafanyakazi wa nyumba za kulala wageni, mashirika ya kidini kama vile BAKWATA, taasisi za kidini kama vile shule za msingi na za sekondari, vituo vya utafiti, ashirika mateule makuu na muhimu ya mawakala wa uwezeshaji na kimkoa, madiwani na kata na wakuu wa idara za kilimo, elimu na utawala wa wilaya za Kyela, Chunya, Mbarali na Mbozi.
Fatma Mrisho Mwenyekiti Mtendaji
SURA YA KWANZA MAONI NA YALIYOBAINIKA
1. Washikadau na vikundi vya walengwa
n Vikundi vya vijana n Wanawake n Walemavu
n WatotoYatima na Waishio katika Mazingira Magumu n Kanisa la Katoliki la Mbeya
n Dayosisi ya Nyanda za Juu za Kusini ya Kanisa la Anglikana n Watu waishio na Virusi vya UKIMWI na/au UKIMWI n Wafanyakazi wa Biashara ya Ngono
n Wahudumu wa Mabaa n Madereva wa Malori
1. 1. Vikundi vya vijana
Ushiriki wa vijana ulikuwa ni mchangamfu na wenye kuzaa matunda katika majadiliano wakati wa ziara ya ufuatiliaji. Walisema wazi wazi kwamba ongezeko la haraka la watu, uhamiaji wa watu kutoka vijijini kwenda mijini, matumizi mabaya na ya mara kwa mara ya pombe, matatizo katika familia, umaskini – kipato kidogo, ukosefu wa ajira kwa vijana, mavazi yanayoamsha hisia za kutaka kufanya ngono, msukumo wa rika wa kumiliki vitu vya anasa na urahisi wa kupatikana kwa picha za ngono kwa kupitia luninga, mikanda ya video na mtandao ni miongoni mwa vichocheo vya janga. Pia ilitambuliwa kuwa wanafunzi huwa hatarini wanapokuwa njiani kuelekea mashuleni na kwenye vyumba vyao na mabweni bila usimamizi na ulinzi.
Idadi ya vikundi vya vijana wapo makini katika kusambaza elimu kuhusu jinsi ya kuudhibiti UKIMWI kwa kupitia njia mbalimbali, kwa mfano maigizo, michezo ya kuigiza na vichekesho. Lakini walisema kuwa wana tatizo la upungufu wa fedha hususani kulipia gharama za usafiri ili kuboresha miradi na shughuli bunifu zao.
Katika kundi hili mambo yafuatayo yalidhihirika:-
n Mavazi yanayoamsha hisia za ngono kama vile “ vimini,” “kk” na “vitopu”
n Wanawake wamechangamka sana katika biashara na ni wepesi n Kutokujuana hali ya afya hususan kuhusu Virusi vya UKIMWI na UKIMWI
baina ya washiriki katika tendo la ngono n Kipato kidogo cha wanawake na wasichana
n Ushindani wa wanawake kwa sababu ya kutumia ngono kama chanzo cha kipato
n Ukosefu wa uaminifu baina ya wanandoa
n Ngono kinyume cha maumbile ilikuwa ni kawaida.
n Wanaume walikuwa tayari kulipa hadi Tshs 50,000 ili kufanya ngono bila kondomu
n Kondomu zilikuwa zinapatikana kirahisi katika mabaa lakini sio kondomu za kike
n Wasichana wengi walikuwa ni wazazi pekee wenye watoto kadhaa. Wateja wanapowaahidi mapenzi au ndoa na kuwa wageni wa mara kwa mara, wanakuwa sio makini na waangalifu.
n Baadhi hawakuwa na chanzo kingine cha kipato na kulazimika kufanya kazi kwenye mabaa. Walieleza haja ya kupatikana kwa kondomu za kike
n Baadhi ya wasichana wanaofanya kazi kwenye baa walisema wanapata mshahara wa Tshs. 15,000 kwa mwezi. Hawakuruhusiwa kujadili kuongezwa mshahara, lakini waliruhusiwa kuchukua zawadi kutoka kwa wateja.
n Kuna umuhimu mkubwa sana wa kuwajengea wanawake uwezo wa kiuchumi ili kupunguza utegemezi kwa wanaume.
1.3. Walemavu
Ukosefu wa habari kuhusu maambukizo ya UKIMWI ulionekana katika kikundi cha walemavu. Walisema hawakuona maana yoyote katika kwenda kupima UKIMWI kwa sababu hawakuona maana yoyote ya kuwapa ushauri watu waishio na Virusi vya UKIMWI na UKIMWI kuboresha mlo wao wakati wao ni maskini. Kikundi hiki kilisema kuwa hakuna afua au afua za kutosha zinazowalenga wao, wakati wanaume huwatongoza wasichana walemavu kwa imani kuwa hawana Virusi vya UKIMWI na UKIMWI. Na
1.4. Watoto Yatima na Waishio katika Mazingira Magumu
Ilionekana kuwa kulikuwa na ongezeko kubwa la watoto yatima na waishio katika mazingira magumu katika jamii. Kila wilaya ina asasi zinazosaidia watoto yatima na waishio katika mazingira magumu. Kwa mfano Kyela kuna asasi ya Oaktree, inayosaidia watoto yatima na waishio katika mazingira magumu kwa kuwapatia misaada ya sare za shule, vitabu, ada za shule, elimu ya ufundi, shughuli za kutengeneza kipato na tiba ya afya. Lakini upeo wa huduma hizi ni mdogo, na wanaonufaika ni wachache. Asasi zingine zinazosaidia watoto yatima na waishio katika mazingira magumu katika wilaya ya Kyela ni Kituo cha Mtakatifu John Hus na USACA, inayohudumia watoto yatima na waishio katika mazingira magumu 521. Zifuatazo ni baadhi ya shughuli zilizopangwa katika
kata 17.
Walitambuliwa watoto yatima na wanaoishi katika mazingira magumu 4370, wanawake 2622 na wanaume 1748, kati yao 1710 wana umri chini ya miaka 5.
n Kuratibu usambazaji wa vifaa ya shule kwa watoto yatima na wanaoishi katika mazingira magumu 524
1.5. Kanisa la Katoliki la Mbeya
Kanisa lina padri aliyeteuliwa kuwa mratibu wa shughuli zinazohusiana na Virusi vya UKIMWI na UKIMWI na anaratibu shughuli za UKIMWI katika parokia 30 ndani ya dayosisi. Afua za sasa hivi zinahusisha ushauri nasaha na upimaji wa hiari, matunzo ya nyumbani na utoaji wa dawa za kuongeza kinga ya mwili, na zinaendeshwa na hospitali za misheni na wafanyakazi wa afya. Kanisa linakutanisha na kuhamasisha vikundi vya vijana na watu wazima kwa kupitia mtandao wake na kulea watoto yatima na wanaoishi katika mazingira magumu 47. Pia wanaandaa shughuli za uelimishaji kwa kutumia burudani katika mashule. Na wanalizungumzia suala la UKIMWI wakati wa mahubiri. Kanisa la Katoliki lipo kimya kuhusu suala la matumizi ya kondomu. Hawairuhusu wala hawaikatazi. Badala yake, wanahamasisha maisha ya kikatoliki yanayosisitiza kusubiri na kuwa mwaminifu.
1.6. Dayosisi ya Nyanda za Juu za Kusini ya Kanisa la Anglikana. Mambo yaliyodhihirika katika eneo hili ni kama ifuatavyo:
v Kanisa linatoa elimu ya kudhibiti UKIMWI, matunzo na tiba na kupunguza athari zitokanazo na UKIMWI ndani ya dayosisi. v UKIMWI unaongezeka Mbeya kwa sababu zifuatazo:-
n Mbeya inapakana na Malawi na Zambia
n Ushindani wa wasichana kwa sababu ya ngono kutumiwa kama chanzo cha kipato
n Ulevi
n Ndoa za mitala
n Ukosefu wa uaminifu baina ya wanandoa n Kipato kidogo cha wasichana na wanawake n Uvaaji wa vimini
Mapendekezo:-n Kampeni ya kuhamasisha Ushauri Nasaha na Upimaji wa Hiari iendelezwe kwa vile inafanikiwa
n Jamii ihamasishwe kuwasaidia watoto yatima na kuelimishwa
n Uendelezaji wa mbinu endelevu kwa ajili ya afua ambazo zinasaidiwa na wafadhili
n Wahudumu wa baa waunde vikundi ili kujenga mshikamano katika mapambano dhidi ya VVU/UKIMWI
n Afua za VVU/UKIMWI zilenge watoto na haja ya kuwa wazi katika majadiliano na mashauri pamoja nao kuhusu VVU/UKIMWI ni muhimu n Afua za VVU/UKIMWI zinazovuka mipaka ya kimataifa zizingatiwe na
kuhusisha washika dau wakiwemo viongozi wa dini
n Uelimishaji kuhusu VVU/UKIMWI hususan matumizi ya kondomu kwa ajili ya viongozi wa dini
1.7. Watu Waishio na Virusi vya UKIMWI na/au UKIMWI
Watu wanaoishi na Virusi vya UKIMWI na UKIMWI wanaelewa vyema vichocheo vya janga, vikiwemo idadi kubwa ya wahamiaji na wasafiri, ukaribu wa mipaka na nchi tatu (Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, Malawi na Zambia), ulevi wa kupindukia, mila na desturi (kwa mfano kurithi wajane), ngono hatarishi na ukosefu wa habari kuhusu VVU/UKIMWI.Uelimishaji na uhamasishaji ni muhimu sana katika kulishughulikia suala hili kiusahihi
Msaada wa kifedha na kiufundi unahitajika sana, kwa mfano baiskeli kwa ajili ya matunzo ya nyumbani na uhamasishaji wa jamii ili kupambana na janga, udumishaji wa huduma bora kwa watu waishio na VVU/UKIMWI na kuwahusisha katika ugharabaishi, kujenga uwezo, kupambana na ubaguzi kutoka kwa wafanyakazi wa afya, na mfuko wa jamii ulioundwa na wilaya. Kwa ujumla ilionekana kuwa watu waishio na VVU/ UKIMWI walitegemea msaada wa mali lakini hawakuzielewa taratibu za ugawaji wa pesa zinazotumiwa na TACAIDS ili kupata msaada wa kifedha. Kwa hiyo elimu zaidi kuhusu upatikanaji wa fedha kwa watu waishio na VVU/UKIMWI inahitajika ili kuwawezesha kubadili mtazamo wao kuwa wa
Kutokujuana hali ya afya kuhusu VVU/UKIMWI baina ya washiriki wa tendo la ngono, na kutotambua na kujadili hali zao za afya kuhusu VVU/ UKIMWI huababisha watu waishio na VVU/UKIMWI kujinyanyapaa na kuacha kutumia dawa za kuongeza kinga ya mwili kwa sababu mbalimbali kama vile dawa kuwafanya watu waishio na VVU/UKIMWI kuwa wachovu kutokana na ukali wa dawa, ukosefu wa milo ya mara kwa mara na ya uhakika, na kadhalika. Kwa hiyo, elimu zaidi inahitajika kwa watu waishio na VVU/UKIMWI kuhusu VVU/UKIMWI na jinsi utumiaji mbaya wa huduma za dawa za kuongeza kinga za mwili unavyoathiri maisha yao.
Pia imani za baadhi ya watu waishio na VVU/UKIMWI na baadhi ya makanisa zinasisitiza kutotumia kondomu na kusitisha huduma za dawa za kuongeza kinga ya mwili kwa watu waishio na VVU/UKIMWI kwa sababu wameokoka (kwa mfano Asemblies, Pentekoste ya Ilemi, Kwambogo, Winners), na kusisitiza kwao kuwa hakuna lisilowezekana kwa jina la Yesu Kristo hujenga imani potofu na tabia mbaya.
1.8. Wafanyakazi wa Biashara ya Ngono
n Makasini Bar wana vipindi vya uelimishaji rika vya afya wakati Nyasanga Bar hawana.
n Wafanyakazi wa mabaa waunde vikundi kujenga mshikamano katika kudhibiti UKIMWI
n Kuna utumiaji mkubwa wa kondomu katika baadhi ya sehemu na utumiaji mdogo katika sehemu zingine
n Upatikanaji wa vifaa vya uelimishaji na kondomu za bure
n Baada ya kufanya kazi kwa muda mrefu katika mabaa wanakuja kuizoea na inakuwa ngumu kwao kubadilika na kufanya kazi nyingine tofauti. n Iligundulika kuwa idadi kubwa ya wateja wao ni madereva wa safari
ndefu wa kitanzania na wachache ni Wamalawi na Wazambia.
n Madereva wa Kizambia na wa Kimalawi hawapendi kutumia kondomu .
n Idadi kubwa ya madereva wa safari ndefu wa Kitanzania hupendelea ngono kinyume na maumbile
n Wagoni wa muda mrefu hawatumii kondomu wakati wote.
n Ugumu wa hali ya uchumi huwalazimisha kufanya vitendo hatarishi vya ngono kwa sababu wanalipwa Tshs 15,000/= tu kwa mwezi
n Kwa sababu ya hali ya hewa ya ubaridi wanahitaji watu wa kulala nao n Ukosefu wa usalama kutokana na fujo na vurugu kutoka kwa wamiliki
1.9. Wahudumu wa Mabaa
Wahudumu wa mabaa walielewa umuhimu wa matumizi ya kondomu na hutembea nazo na kuwavalisha wateja wao, lakini walisema kuwa baadhi ya wateja, hasa kutoka Malawi, waling’ang’ania kufanya ngono bila kondomu Vitendo vya Ngono kinyume na maumbile vilikuwa ni kitu cha kawaida. Wanaume walikuwa tayari kulipa hadi Tshs. 50,000 kwa ajili ya kufanya ngono bila kondomu.
Kondomu zinapatikana kiurahisi katika mabaa lakini sio kondomu za kike. Wasichana wengi walikuwa ni wazazi pekee wenye watoto kadhaa. Wateja wakiwaahidi mapenzi au ndoa na kuanza kuwa wageni wa mara kwa mara, wanajisahau na kupoteza umakini. Baadhi yao hawakuwa na chanzo kingine cha kipato na hivyo kulazimika kufanya kazi baa. Walieleza umuhimu wa kondomu za kike kuwa rahisi zaidi kupatikana.
1.10. Madereva wa Malori
Madereva wa malori walisema kuwa, kwa sababu ya uwezo mdogo wa vivuko vya mpakani kama vile Tunduma na Kasumulo walilazimika kukaa siku nyingi katika vitongoji viliyopo barabarani na viliyojaa watu kama Mbeya, Kyela, Kasumulo na Tunduma kusubiri huduma katika vivuko vya mipaka. Madereva wa malori wanatumia muda wao mwingi sana katika unywaji wa pombe na kukimbizana na wasichana wanaowafuata kwa sababu ya pesa zao.
Imani ya kuwa madereva wa malori wanabeba pesa nyingi imesababisha idadi kubwa ya wafanyakazi wa biashara ya ngono kuwafuata katika vitongoji hivyo vyenye msongamano wa watu wengi.
Utafiti ulionyesha kuwa ni madereva wa lori wachache wanaotumia kondomu wanapofanya vitendo vya ngono na wafanyakazi wa biashara ya ngono.
n Ulevi wa kupindukia
n Ufahamu mdogo kuhusu Virusi vya UKIMWI na UKIMWI n Mila na desturi hatarishi
n Unyanyapaa na ubaguzi
n Uhamiaji wa watu kutoka vijijini kwenda mijini
n Barabara kubwa na mipaka baina ya nchi tatu (Zambia, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo na Malawi)
n Sherehe na shughuli za kukesha (Mbio za Mwenge, ngoma, misiba na unyago)
n Imani potofu na za uongo kuhusu Virusi vya UKIMWI na UKIMWI n Matumizi yasiyo ya wakati wote ya kondomu
n Uwezo mdogo wa vivuko vya mpaka (Tunduma na Kasumulo) unaosababisha msongamano wa watu, magari na mizigo Tunduma, Kasumulo, Kyela na Mbeya.
n Ukosefu wa ajira unaosababisha vikundi vya vijana vinavyojulikana kwa jina la mtaani kama “vijiwe”
n Mavazi yanayoamsha hisia za kutaka kufanya kitendo cha ngono (kwa mfano vimini, bikini nk)
n Kuruhusiwa kuingia na kuhudumiwa kwa wavulana na wasichana wadogo katika mabaa, nyumba za kulala wageni na vituo vingine vya starehe na burudani
n Picha za ngono katika redio, luninga na mtandao
n Tabia hatarishi za wafanyabiashara kutoka sehemu mbalimbali za nchi.
n Ongezeko la vitendo vya ubakaji (Chunya) n Uwepo wa migodi (Chunya)
n Kuajiriwa kwa wasichana wadogo (chini ya umri wa miaka 18) katika mabaa na vituo vya starehe na burudani.
n Hali ya hewa ya ubaridi ya Mbeya pia imeelezwa kuwa ni moja ya sababu za ongezeko la kasi ya maambukizo ya Virusi vya UKIMWI na UKIMWI n Ushindani kati ya wasichana kutokana na ngono kutumiwa kama njia
ya kupata pesa. n Ndoa za mitala
n Ukosefu wa uaminifu katika ndoa n Urithi wa wajane
3.0. Takwimu Mbalimbali Jedwali la 1
3.1. Takwimu za Mkoa wa Mbeya
1. Idadi ya Watu 2,070,041
Wanaume: 990,820 Wanawake: 1,079,221
2. Kasi ya maambukizo 13.5%
3. Kasi ya maambukizo
kutoka kwa mama kwenda kwa watoto
12.7%
4. Vituo vya Ushauri
Nasaha na Upimaji wa Hiari
133
5. Vituo vya Matunzo na
Tiba (15 za zamani, 32 mpya)
6. Kamati za Kudhibiti UKIMWI za Serikali za
Mitaa Zipo wilaya zote lakini zinatofautiana ufanisi
7. Matumizi ya Kondomu Tazama Taarifa ya Idadi ya Watu na Afya
8. Kasi ya maambukizo (Magonjwa ya Zinaa) 2.5%
9. Idadi ya Wilaya 8 10. Majina ya Wilaya 1. Mbeya mjini 2. Mbeya vijijijini 3. Chunya 4. Mbozi 5. Ileje 6. Mbarali 7. Rungwe
12 Majina ya Mamlaka za
Wilaya Wakuu wa Wilaya 1. Chunya: Fatuma Kimaryo
2. Ileje: Esther Wakali
3. Kyela: Hussein H. Mashimba 4. Mbarali: Hawa Ngulume 5. Mbeya Mjini na Mbeya Vijijini: Leonidas Gama
6. Mbozi: Hamali Kihemba 7. Rungwe: Mariam Mgaila Makatibu Tawala wa Wilaya 1. Mbeya Mjini: Elizabeth Mnuo 2. Mbeya Vijijini: Juliana Mayange 3. Chunya: Maurice Sapanio 4. Ileje: Yona L. Maliki
5. Mbarali: George Kagomba 6. Mbozi: Livistone Siliowa 7. Kyela: S.P. Linuma
8. Rungwe: M.E.M Buliga
13. Wakala wa Uwezeshaji
wa Kimkoa GTZ International Services
14. Kiongozi wa timu ya
Wakala wa Uwezeshaji wa Kimkoa
Dr. Bruno Masumbuko
15. Idadi ya Vikundi vinavyo
hudumiwa na wakala wa uwezeshaji wa kimkoa
Jumla 84, 47 zenye kuwahi kuwa na mkataba na 37 zenye mikataba mipya.
16. Kiasi kilichotolewa na
TACAIDS katika Mkoa wa Mbeya bila kupitia wakala wa uwezeshaji wa kimkoa
2005/2006:
2006/2007: Tshs: 6,100,000 hii idadi
haihusishi pesa zilizotolewa kwa Halmashauri za wilaya
17. Jina la mwakilishi wa
NACOPHA Nd.Grace Mwahongo
18. Kiasi kinachotolewa
kwa Mkoa na Wilaya kila mwaka
Misaada kutoka Mfuko wa Mwiitikio wa Jamii kuhusu UKIMWI kwa Vyama vya Kiraia na Mfuko wa Pamoja wa Jamii kwa 2005/6
Wilaya TShs kwa vyama vya kiraia TShs kwa Mfuko wa Pamoja wa Jamii 1.Rungwe 2.Kyela 3. Mbeya mjini 4. Mbeya vijijini 5. Mbarali 6. Chunya 7. Ileje 8. Mbozi Jumla 30,837,500 28,741,000 32,238,100 23,755,110 34,077,400 34,500,000 26,020,000 40,662,076 250,833,586 2,000,000 2,000,000 2,000,000 2,000,000 1,500,000 2,000,000 1,996,500 2,372,000 15,868,500 19. Aina za utafiti unaofanyika katika mkoa
1. Utafiti wa Majaribio ya Kinga 2. Ukaguzi wa zamu
3. Ubora wa huduma za kutibu magomjwa ya zinaa
4. Utafiti wa Maendeleo ya Mgonjwa 5. Utafiti wa Maambukizi
6. Utafiti wa tiba za kuongeza kinga 7. Utafiti wa kifua kikuu
20. Asasi zinazoshiriki 1. GTZ (TGPSH) 2. Water Reed 3. PSI 4. CARITAS 5. Abbot Fund 6. LCCB AMREF 21. Lengo la Mfumo wa Matumizi la Katikati ya Muhula wa Mbeya
Kuboresha huduma na kupunguza kasi ya maambukizo ya UKIMWI ifikapo 2010
3. 2 Takwimu za Wilaya ya Mbeya
Idadi ya watu katika wilaya ya Mbeya kwa jinsia na umri.
Umri/Rika Wanaume Wanawake Jumla
80+ 882 1,074 1,956 75 – 79 773 807 1,580 70 – 74 1,273 1,532 2,805 65 – 69 1,428 1,927 3,355 60 – 64 2,008 2,795 4,803 55 – 59 2,038 2,489 4,527 50 – 54 2,718 3,727 6,445 45 – 49 3,251 4,237 7,488 40 – 44 4,297 5,218 9,515 35 – 39 5,373 6,555 11,928 30 – 34 6,990 8,411 15,401 25 – 29 8,804 11,483 20,281 20 – 24 9,332 13,597 22,929 15 - 19 13,553 14,416 27,969 10 - 14 16,846 17,380 34,226 5 - 9 18,825 19,272 38,097 0 - 4 20,405 20,552 40,957 Jumla 118,597 135,472 254,069
Jedwali la 3
Idadi ya Watu Kwa Kata Katika Wilaya ya Mbeya
Na. Jina la Kata Idadi ya Vijiji Idadi ya Kaya Idadi ya Watu Jumla Wanaume Wanawake 1 IHANGO 5 2,855 5,280 5,910 11,190 2 ULENJE 7 3,081 5,178 6,295 11,473 3 TEMBELA 11 3,836 6,604 8,056 14,660 4 IJOMBE 7 2,439 4,081 4,857 8,938 5 SANTILYA 7 3,937 6,926 8,291 15,217 6 ILEMBO 13 5,173 10,082 11,718 21,800 7 IWIJI 5 3,091 6,188 7,077 13,265 8 ISUTO 11 5,275 9,649 11,337 20,986 9 IGALE 9 4,485 8,259 9,628 17,887 10 IWINDI 8 3,789 7,151 8,147 15,298 11 UTENGULE USONGWE 7 10,740 20,897 23,192 44,089 12 MSHEWE 8 2,482 5,230 5,374 10,604 13 IKUKWA 2 1,240 2,375 2,703 5,078 14 IYUNGA MAPINDUZI 5 1,479 2,758 3,043 5,801 15 BONDE LA SONGWE 6 3,953 8,061 8,301 16,362 16 INYALA 8 2,780 5,180 5,923 11,103 17 ILUNGU 7 2,887 4,901 5,417 10,318 JUMLA 126 63,522 118,800 135,269 254,069
Vifaa vya Uelimishaji
Taarifa ya vifaa vya Uelimishaji Jan –Des 2006
Vifaa Salio Zimepokelewa Jumla Zimesambazwa Salio
Vipeperujshi - Matumizi ya kondomu 34325 31600 65925 50400 15525 Vipeperushi - STD 24525 32000 56525 45900 10625 Vipeperushi - VCT 23097 32000 55097 44700 10397 Vipeperushi - ARV 32808 32000 64808 40700 24108 Vipeperushi - PMTCT 22408 31000 53408 38600 14808 Vipeperushi - PMTCT 29258 31000 60258 37870 22388
Vitabu - Maswali na Majibu 4799 7350 12149 8680 3469
Vitabu 8 908 5000 5908 5117 791
Vitabu 570 0 570 310 260
Vitabu - Kuelewa kuishi na
VVU 7808 0 7808 3480 4328
Vitabu – PHEs guide STD V 164 1000 1164 906 258
Vitabu – PHEs guide STD VI 84 1000 1084 906 178
Vitabu - PHEs guide STD VII 1340 0 1340 916 424
Mikanda ya video 129 0 129 9 120
Vipeperushi 0 15000 15000 12030 2970
Vipeperushi - Hope for
Tanzania Part I 91 0 91 17 74
Vikpeperushi - Hope for
Tanzania Part II 56 0 56 17 39
Vipeperushi - Wasichana
kama hutaki mimba 0 15000 15000 13650 1350
Mabango 2920 0 2920 1672 1248
Mabango - Ishi upendavyo 0 2000 2000 96 1904
Mabango - Bill boards 0 16 16 16 0
Mabango - Huwezi
kutambua VVU Mabango 0 2000 2000 96 1904
Mabango - Unyanyapaa 0 4000 4000 2900 1100
Vipeperushi 0 6000 6000 5800 200
Fulana na Kofia 0 0 0 0 0
Chanzo : Taarifa ya VVU/UKIMWI na magonjwa ya zinaa ya Mradi wa Kudhibiti UKIMWi ya Mkoa wa Mbeya - 2006
Jedwali la 5
3.4 Elimu Rika
a) Shule za Msingi
Wilaya Idadi ya Shule Shule zenye elimu rika Maelezo zaidi ya ziada
Mbeya Rural 125 76 Msaada mwingi kutoka TGPSH
Rungwe 196 44 Msaada mwingi kutoka TGPSH
Mbozi 202 13 Msaada mwingi kutoka TGPSH
Chunya 101 53 Msaada mwingi kutoka TGPSH lakini pia kutoka kwenye jamii
Ileje 83 0 Hamna mafunzo yaliyoendeshwa
Mbarali 102 0 Hamna mafunzo yaliyoendeshwa
Kyela 99 0 Uhamasishaji umefanyika kwa walimu na kamati katika shule
kumi tu
Mbeya Urban 75 51 Msaada mwingi kutoka TGPSH
Jumla 983 237
Katika shule nyingi elimu rika hutolewa kuanzia darasa la tano
Ongezeko la shule za msingi zisizo kuwa na elimu rika Mkakati madhubuti ni muhimu kwa ajili ya uendelevu
Chanzo: Taarifa ya VVU/UKIMWI na magonjwa ya zinaa ya Mradi wa Kudhibiti UKIMWi ya Mkoa wa Mbeya - 2006
b) Maeneo yenye kasi kubwa ya Maambukizo
Wilaya Idadi ya maeneo
yenye kasi kubwa ya maambukizo
Maeneo yenye kasi kubwa ya maambukizo yenye elimu rika
Idadi ya waelimishaji rika Mbeya Vijijini 10 10 20 Rungwe 10 10 20 Mbozi 10 10 14 Kyela 3 3 6 Chunya 4 4 8 Ileje 3 2 4 Mbarali 4 4 8 Mbeya Mjini 14 10 20 Jumla 52 50 100
Chanzo: Taarifa ya VVU/UKIMWI na magonjwa ya zinaa ya Mradi wa Kudhibiti UKIMWi ya Mkoa wa Mbeya - 2006
Jedwali la 7 (c) Afua Makazini
Wilaya Idadi ya maeneo ya kazi Idadi ya maeneo ya kazi zenye elimu rika ya afya
Mbeya Vijijini 6 4 Rungwe 6 1 Mbozi 15 15 Chunya 5 4 Ileje 4 3 Mbarali 5 0 Kyela 5 3 Mbeya Mjini 13 8 Jumla 59 38
Jedw ali la 8 a k ondomu Mauz o kw a k at oni Jumla y a ka toni Mar . Apr . Mei. Jun. Jul. Ag o. Sep . Okt. No v. Des. 154 286 435 60 451 582 766 217 330 195 4425 13 0 65 0 0 22 56 12 11 22 283 44 33 33 33 22 70 24 56 68 77 514 0 24 70 77 44 44 113 55 39 88 631 10 26 0 33 35 44 56 22 62 22 322 66 54 94 22 55 339 0 156 44 33 894 22 33 88 0 0 55 23 0 113 11 389 66 20 11 22 11 25 11 8 9 11 209 375 476 796 544 618 1181 937 529 678 459 7918 216000 27 4176 458496 313344 355968 680256 539712 304 704 390803 264384 4,561, 043 a bur e ,909 o sambazw a: 6, 005 ,952 a y a zinaa y a Mr adi w a K udhibiti U KIM W i y a Mk oa w a Mbe ya - 2006
3.6 Idadi ya wagonjwa wa UKIMWI katika makliniki 1. Igogwe 62 2. Isoko 25 3. Kyela 430 4. Matema 198 5. Mbalizi 160 6. Mbarali 8 7. Mbeya Regional 3 8. Mbozi Mission 54 9. Mwambani 311 10. Tukuyu 50 11. Uyole 106 Jumla 1,407
Chanzo: Taarifa ya VVU/UKIMWI na magonjwa ya zinaa ya Mradi wa Kudhibiti UKIMWi ya Mkoa wa Mbeya - 2006
Jedw ali la 10 a Virusi v ya U KIM W I k ut ok a kw a Mama kw enda kw a Mt ot o a Hiari K atik a Kliniki za o Chunya Ileje Kyela Mbarali Willaya y a Mbeya t Mji wa mbeya Mbozi Rungwe Jumla 2 2 1 1 4 8 3 8 29 1939 585 1522 1119 2424 11,573 3358 3882 26, 402 1969 609 1666 1037 1763 5906 226 7 3926 19, 143 1594 434 1571 943 1569 5076 1817 3903 16,907 1594 434 1570 910 1566 5071 1815 3902 16,862 KIM WI 189 26 248 148 230 711 200 393 2145 50 8 83 69 122 269 116 249 966 a kinga 0 0 0 0 0 1036 67 35 1138 100 10 48 32 63 169 69 197 688 98 10 48 32 63 151 63 188 653 12 0 17 8 18 27 16 37 135 2058 808 1663 1733 1010 11,301 4368 2964 25,905 622 184 695 257 372 1599 695 1410 5834 0 0 0 0 0 340 8 5 353 66 11 79 62 22 351 105 264 960 65 11 136 62 26 434 106 264 110 4 63 10 122 61 21 350 103 241 971 usudiw a k un yon yesha 74 10 120 61 24 416 106 261 1072
utoa huduma mbadala
1 1 16 1 2 18 0 8 47 0 0 0 0 0 73 12 0 85 0 0 0 0 0 21 0 0 21
ya virusi vya UKIMWI kutoka kwa mama kwenda kwa motto, 17 walikuwa na VVU na/au UKIMWI (Taarifa ya VVU/UKIMWI na magonjwa ya zinaa ya Mradi wa Kudhibiti UKIMWi ya Mkoa wa Mbeya - 2006 Jedw ali la 11 onjw a y a Zinaa GU D GDS PI D RPR CHANY A MENGI NEY O KU KU TANA JU ML A JU ML A KUU -Me -K e -Me -K e -K e -Me -K e -Me -K e -Me -K e -Me -K e 751 810 725 1049 1113 157 379 148 286 757 707 2538 4344 6882 235 248 236 324 353 66 138 3 71 163 16 7 703 1301 2004 485 474 466 649 526 70 187 88 139 34 6 324 1455 2299 3754 434 369 513 571 516 113 177 88 105 308 348 1456 2086 3542 602 521 645 821 772 123 273 128 169 525 513 2023 3069 5092 492 514 54 6 689 577 123 310 308 150 432 385 1901 2625 4526 86 7 894 939 1234 1210 222 452 183 273 74 6 684 2957 47 47 7704 639 64 7 723 922 1091 213 416 114 227 597 578 2286 3881 616 7 4,505 4, 477 4, 793 6,259 6, 158 1,087 2,332 1,060 1,420 3,87 4 3,706 15 ,319 24 ,352 39,6 71 a y a VV U/U KIM WI na magonjw a y a zinaa y a Mr adi w a K udhibiti U KIM W i y a Mk oa w a Mbe ya - 2006
Jedw ali la 12 tunz o y a Nyumbani W anaume w aliopima W anaw ak e w aliopima Jumla W anaume Chan ya W anaw ak e Chan ya Jumla Chan ya 332 381 713 209 233 442 16,226 20 ,590 36,816 4, 025 6,227 10 ,252 653 16,907 17,560 135 2,145 2,280 17 , 211 3 7,8 78 55,089 4,369 8,605 12,9 74 a y a zinaa y a Mr adi w a K udhibiti U KIM W i y a Mk oa w a Mbe ya - 2006
Jedw ali la 13 Ma tunz o y a Nyumbani a Idadi y a Mk oa: W ag onjw a w ap ya 4 ,5 90 , w a zamani 3, 415. Jumla 8,005 Jumla y a vituo v ya afy a W aliosimamiw a 25 18 46 23 37 17 ila yani 39 21 35 19 55 22 47 20 24 9 340 149 a y a VV U/U KIM WI na magonjw a y a zinaa y a Mr adi w a K udhibiti U KIM W i y a Mk oa w a Mbe ya - 2006
Jedw ali la 14 Ky ela Mbar ali Ma tema Vw aw a Isok o Uhai MRH Regional Rungw e JWT Z Ig ogw e Mw ambani Jumla kwa Mkoa tiba 289 119 77 704 4 0 1537 634 572 216 245 142 5156 899 46 129 1154 9 0 2694 1265 84 7 355 175 7657 96 68 4 107 0 518 106 118 18 8 1058 ya k uongez a kinga y a m wili 827 5 44 273 4 740 366 237 80 74 81 2773 394 9 41 335 9 1207 686 24 7 74 100 92 3265 53 0 3 23 0 256 44 45 6 9 0 442 a kinga y a m
wili lakini haw
ajaanz a 178 7 17 156 0 126 19 92 5 4 61 701 217 13 14 257 3 175 79 127 8 6 83 1033 108 0 1 34 0 36 12 38 6 0 8 256 a y a zinaa y a Mr adi w a K udhibiti U KIM W i y a Mk oa w a Mbe ya - 2006
CHANGAMOTO
Kuna halmashauri nane katika Mkoa wa Mbeya, ambapo mkoa mzima
una wadau wanaoziratibu katika masuala yote yanayohusiana na VVU/UKIMWI. Wakati wa ziara ya timu kutoka TACAIDS ilitambulika kuwa halmashauri kwa kiwango fulani hazitekelezi kazi vyema ipasavyo katika suala zima la kupambana vita dhidi ya VVU/UKIMWI katika mkoa. Hii ilionekana wakati wa majadiliano ambapo mipango ya halmashauri ilihusisha shughuli za VVU/UKIMWI lakini inatekelezwa polepole. Sababu kuu ni ucheleweshaji wa malipo ya pesa wanazogawiwa kwa ajili ya shughuli za VVU/UKIMWI.
Kwa hiyo waratibu wa UKIMWI wa Halmashauri za Wilaya walisisitiza kuzihamasisha halmashauri. Hii inatajwa katika tafiti iliyofanywa Mbeya na Dr.Ulrich F. Vogel chini ya mradi wa UNAIDS mnamo Machi, 2007. Kama alivyoonyesha na ilivyojadiliwa mnamo 2005 wakati wa warsha ya kitaifa, kamati za kudhibiti UKIMWI katika mamlaka za serikali za mitaa zilishutumiwa kwa kuwa wazito na kuona UKIMWI kama “biashara kama kawaida” na pia kukosa uongozi na ari.
Hata hivyo, licha ya hizi shughuli kipande kikubwa cha jamii hakijafikiwa. Kwa hiyo maelezo kuhusu maambukizi ya UKIMWI katika jamii ya wafuga ng’ombe wa kimasai na waendesha tohara wa kijadi (ngariba) hayajulikani.
Kumekuwa na ongezeko la huduma za VVU na UKIMWI. Upatikanaji wa elimu inayofaa na sahihi kuhusu UKIMWI unaendelea kuwa changamoto. Ingawa wafanyakazi wa biashara ya ngono wanatambulika kuwa ni moja ya vichocheo vikuu vya janga, kuna miraddi michache sana inayowalenga wao.
Kuna mafunzo mengi muhimu yaliyopatikana kutokana na miradi mbalimbali katika mkoa, lakini mingi haiwekewi kumbukumbu wala haihadithiwi.
Changamoto
n Ugumu wa kupata taarifa hasa kutoka Hospitali ya Rufaa ya Mbeya kwa mfano taarifa kwa ajili ya watoaji damu na wagonjwa wa UKIMWI.
n Idadi kubwa ya watu waishio na VVU/UKIMWI wanaostahili tiba za kuongeza kinga ya mwili lakini hawaipati.
n Usimamizi usiokuwa wa mara kwa mara
n Upimaji wa kaswende wa mama wajawazito bado hautoshelezi kwani kuna vituo 77 vya afya vyenye uwezo wa kupima wajawazito kati ya vituo 340.
kubwa ya maambukizi, na wafanyakazi wa afya wenye kufanya kazi za ziada. n Ukosefu wa uhakika katika utengenezaji na usambazaji kutoka Duka la Vifaa vya
Afya
n Uwezo mdogo wa maafisa maendeleo wa kata kutekeleza shughuli za maendeleo katika kata. Hii inasababishwa na upungufu wa pesa za kuendesha mafunzo ya wafanyakazi.
n Uwezo mdogo wa kusimamia na kufuatilia harakati za kupambana na UKIMWI katika ngazi ya kata.
n Uhusishaji mdogo wa maafisa maendeleo na mashirika yanayofanya kazi katika Manispaa ya Mbeya.
n Ukosefu wa usafiri wa kuaminika kwa wafanyakazi kwani kuna kata 36 katika wilaya ya Mbeya vijijini.
n Mchanganyiko wa watu masokoni, viwandani, kwenye sherehe za kidini na kwenye mabaa.
n Mchanganyiko wa wageni na wasafiri kutoka nchi za jirani kama vile Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, Malawi na Zambia.
n Mimba za wasichana wadogo
n Mila na desturi, kwa mfano kurithi wajane n Kasi kubwa ya maambukizi - 13.5%
n Uimarishaji wa mbinu zilizopo pamoja na mfumo mpya katika ngazi ya mitaa Je, utachangia kupunguza kasi ya maambukizi katika miaka 5 na 10 ijayo?
n Unyanyapaa na ubaguzi n Magonjwa ya zinaa
n Ucheleweshaji wa malipo ya pesa n Kazi nzito kwa wafanyakazi wachache.
MAFANIKIO
1. Elimu rika
Maeneo yanayolengwa ni maeneo yenye kasi kubwa ya maambukizo, sehemu za kazi na shule za msingi. Kwa upande wa elimu rika katika shule za msingi, semina na mafunzo yameendeshwa kwa vikundi vya walengwa. Mafunzo yaliendelea mwaka huu katika baadhi ya wilaya kwa kuanzisha elimu rika katika baadhi ya shule au kwa kuimarisha elimu rika iliyopo sasa katika shule za msingi, ingawa katika uwezo tofauti. Elimu Rika katika sehemu za kazi iliimarishwa kwa mafunzo ya siku 3 ya waelimishaji rika wote kutoka hospitali ya mkoa wa Mbeya. Pia, makampuni binafsi yaliendesha mafunzo chini ya msaada wa kiufundi wa mkoa na ushauri kutoka kwa waelimishaji wa waelimishaji waliopo katika mkoa.
Shughuli mbalimbali zilizokuwa zinaendelea katika maeneo yenye kasi kubwa ya maambukizo tofauti ziliimarishwa na kuendelezwa. Mradi uliendesha mafunzo kwa ajili ya wilaya za Mbeya Mjini na Vijijini kwa watu 39. Mafunzo yalitanguliwa na mkutano wa uhamasishaji kwa wafanyakazi na wamiliki wa mabaa. Ilifuatiwa na mkutano wa kutambulishana baina ya matabibu kutoka maeneo yenye kasi kubwa ya maambukizo na waelimishaji rika waliopata mafunzo,
2. Utengenezaji na usambazaji wa vifaa vya uelimishaji
Kwa njia ya moja kwa moja au vinginevyo mradi huu unafikia jamii na unahitaji vifaa mbalimbali vya uelimishaji ili kuendelea kutoa elimu kwa watu. Jedwali la 4 (Ukurasa wa 10) linaorodhesha aina za vifaa vya elimu ya afya zilizotengenezwa na/au kusambazwa. Vifaa hivyo ni pamoja na vipeperushi, vitabu, kalenda, mabango nk. Matangazo ya redio yaliyotengenezwa na kurushwa hewani hapo awali, yanaendelea kurushwa hewani mwaka huu. Vifaa vya elimu vimekuwa vikitakiwa na kuhitajika sana ndani na nje ya mkoa na vimekubalika katika jamii.
3. Maonyesho ya maigizo na filamu.
Vikundi 5
vilivyosajiliwa vya maigizo vimekuwa vikifanya maonyesho katika maeneo yao lakini vingine kama
KIHUMBE vimekuwa
vikifanya maonyesho hadi nje ya maeneo yao kwa mialiko maalumu. Idadi ya maeneo yaliyoonyesha michezo ya kuigiza ni 275 na yalihudhuriwa na watu 255,123 kutoka katika idadi iliyotegemewa ya watu 305,107.
Maigizo mengine huendeshwa katika maeneo tofauti kwa kutumia vikundi visivyosajiliwa vilivyopo katika kila wilaya. Wilaya
4. Mikutano /Mafunzo/Semina/Warsha
Chini ya kipengele hiki yafuatayo yalitekelezwa:
i) Mafunzo ya siku 5 ya kuendeleza elimu rika katika maeneo yenye kasi kubwa ya maambukizo Mbeya Mjini/Vijijini yaliyoenda sambamba na mkutano wa uhamasishaji kwa wamiliki na wafanyakazi wa mkoa na wanachama wa Kamati ya Kudhibiti UKIMWI ya Kata kutoka maeneo yenye kasi kubwa ya maambukizo;
ii) Kongamano la siku moja la wafanyakazi wa hospitali ya mkoa na familia zao lililofanyika Siku ya Familia duniani,
iii) Mkutano wa UKIMWI wa Arusha 2007;
iv) Uadhimishaji wa siku ya UKIMWI duniani, iliyoadhimishwa kimkoa Kyela; v) Hakuna mafunzo ya kuanzisha elimu rika kwa madereva wa teksi wa mji wa
Mbeya;
vi) Semina za uhamasishaji kwa Timu ya Afya ya Halmashauri ya Wilaya ili kuanzisha elimu rika UKIMWI makazini katika ngazi ya hospitali;
vii) Mkutano wa afya wa mkoa uliofanyika siku tatu kila baada ya miezi mitatu ambapo wanachama wa Timu ya Afya ya Halmashauri ya Wilaya /Timu ya Afya ya Halmashauri ya Mkoa pamoja na wataalamu walikutana kwa lengo la kuboresha na kuimarisha huduma za afya katika Mkoa wa Mbeya. Huu
viii) Utoaji wa msaada wa kiufundi kwa sekta ya umma na binafsi kwa kupitia mafunzo/mikutano katika eneo la Virusi vya UKIMWI/UKIMWI. Warsha iliandaliwa Dar es Salaam kwa msaada wa Mfuko wa Dunia ili kupata taarifa ya maendeleo.
ix) Mkutano na watu wa vyombo vya habari kwa lengo la kuwapatia habari mpya kuhusu Virusi vya UKIMWI/UKIMWI.
5. Uhamasishaji wa Matumizi ya kondomu
Mkoa wa Mbeya una kondomu za bure na zinazouzwa zinazowafikia watu kupitia njia tofauti. Hii ni ili kuhakikisha kuwa kondomu zinapatikana muda wote ili watu wenye kushindwa kusubiri au kuwa waaminifu wapate matumizi sahihi na hakika ya kondomu. Jumla ya idadi ya kondomu zilizosambazwa ni kondomu 6,005,952.
6. Utafiti
Katika kutekeleza lengo lake la kufuatilia nyendo za janga, mradi umejihusisha na tafiti tofauti kwa miaka. Mara kwa mara, mradi umekuwa ukitoa taarifa za wagonjwa wa UKIMWI kwa Mradi wa Taifa wa Kudhibiti UKIMWI na idadi iliyotolewa mwaka huu ya wagonjwa wa UKIMWI ni 1,408. Ukusanyaji wa takwimu unategemewa kuanza Januari, 2007
7. Huduma za Matunzo na Tiba
Huduma hii ilianzishwa Oktoba 2004 katika mkoa. Ujenzi wa uwezo kwa ajili ya wafanyakazi wa afya katika hospitali ya rufaa ya Mbeya uliendelea na vituo vinavyotoa huduma za matunzo na matibabu sasa hivi ni pamoja na hospitali za mkoa na rufaa, hospitali zote za wilaya, hospitali ya misheni ya Igogwe, hospitali ya Kilutheri ya Matema, hospitali na kituo cha Uhai Baptist, hospitali ya Mwambani, hospitali ya Isoko na hospitali ya Chimala. Jumla ya wagonjwa waliohudumiwa ni 13,911; waliopata dawa ya kuongeza kinga ya mwili ni 3,480, na waliotakiwa kupata dawa ya kuongeza kinga ya mwili ni 8,470.
Kupitia uraghibishi na uhamasishaji baadhi ya shughuli zilipata msaada na pesa kutoka Serikali za Mitaa. Shughuli zilizopata msaada wa pesa ni pamoja na usimamizi, elimu rika katika shule za msingi na maeneo yenye kasi kubwa ya maambukizo ya UKIMWI, maigizo na maonyesho ya filamu pamoja na matukio ya kitaifa kama Siku ya Ukimwi Duniani. Juhudi zinaendelea kupata msaada mkubwa zaidi.
10. Uboreshaji wa Usafi wa Vifaa vya Hospitali
Katika kuhakikisha kuwa watu hawapati maambukizo ya VVU kwa kupitia vifaa vya hospitali, vituo vyote vya afya huchemsha vifaa vyake kwa kutumia chombo maalumu cha kuondoa vijidudu vyote vya ugonjwa kwa kuchemsha au kwa kupasha moto. Pia, wafanyakazi wa afya walikuwa wanakumbushwa wakati wote kuhusu uwezekano wa kupata maambukizo wakati wanafanya kazi au uwezekano wa kumwambukiza Virusi vya Ukimwi mgonjwa kutoka kwa mgonjwa mwingine kwa bahati mbaya, hivi karibuni wafanyakazi wote kutoka hospitali ya mkoa ya Mbeya walihudhuria semina ya siku nne iliyohusu jinsi ya kudhibiti maambukizo.
11. Uzuiaji wa maambukizi ya Virusi vya UKIMWI kutoka kwa Mama Kwenda Kwa
Mtoto
Mkoa uliweza kuongeza huduma hadi kuzifikia wilaya zote na jumla ya idadi ya vituo imefika 29 kutoka vituo 4 vilivyokuwepo kabla. Vyote vinasimamiwa mara kwa mara na wanawake wajawazito wanapata huduma ipasavyo. Jumla ya wanawake wajawazito 960 na watoto wachanga 1104 walipata dawa iitwayo “Nevirapine”. Jumla ya wanawake wajawazito waliopata ushauri nasaha na kupima Virusi vya UKIMWI ni 16,907 kati ya wanawake wajawazito 26,402 waliopata huduma ya awali ya kliniki. Wanawake wajawazito 2,145 waligundulika kuwa na virusi vya UKIMWI.
Waume pia wanazidi kuhusishwa. Jumla ya waume 653 walipima na 135 waligundulika kuwa na Virusi vya UKIMWI.
Huduma ya Uzuiaji wa maambukizi ya Virusi vya UKIMWI Kutoka kwa Mama Kwenda kwa Mtoto iliendelea na jumla ya wateja 2,409 walipimwa. 265 walijiandikisha kwenye idadi ya CD4 na 235 wanapata tiba ya vidonge vya kuongeza
kinga ya mwili.
dalili za magonjwa. Mfumo wa kuagiza madawa wa mfumo wa pull umetumiwa mwaka mzima. Lakini bado kuna matatizo katika upokeaji wa bidhaa zilizoagizwa.
13. Ushauri Nasaha na Upimaji wa Hiari na Matunzo ya Nyumbani
Mkoa una vituo vya afya 117 vyenye kutoa huduma ya ushauri nasaha na kupima na jumla ya idadi ya washauri nasaha katika mkoa ni 234. Jumla ya idadi ya wateja walioshauriwa na kupima ni 55,098. Na katika hawa, 12,983 walikuwa na Virusi vya UKIMWI. Matunzo ya nyumbani yanatolewa kwa wateja 8,005. Kwa ujumla kuna idadi inayoongezeka ya watu wanaopata ushauri nasaha na kupima na matunzo ya nyumbani. Jamii nayo inazidi kujihusisha katika kutoa huduma ya matunzo na msaada abayo ni dalili ya kupungua unyanyapaa.
Kuhusiana na ujenzi wa uwezo, watoaji huduma ya matunzo ya nyumbani 80 kutoka katika jamii walipata mafunzo Rungwe na Mbozi kwa msaada wa ufadhili wa Walter Reed.
14. Usalama wa Damu na Maabara
Huduma ya usalama wa damu iliendelezwa na kila kituo cha afya ambapo damu ilipimwa kugundua kama ina Virusi vya UKIMWI. Huduma hii imekuwa ikiongezeka kasi mara kwa mara sambamba na uhamasishaji na uhusishaji wa jamii.
15. Kutembeleana na Matukio
n Nane Nane:- Wakati wa tukio hili Mradi wa kudhibiti UKIMWI Mkoa wa Mbeya (MRACP) waliandaa shughuli tofauti ikiwemo ushauri nasaha na upimaji wa hiari, huduma ya tiba ya magonjwa ya zinaa, uelimishaji, maigizo na maonyesho ya filamu. Jumla ya wateja 1331 walipata huduma za ushauri nasaha na kupima, na 109 waligundulika kuwa na Virusi vya UKIMWI.
MAPENDEKEZO Njia ya mbele:
n Kufuatilia kwa umakini shughuli za asasi zisizo za kiserikali katika ngazi ya kata.
n Shughuli za mapambano dhidi ya UKIMWI zinazotekelezwa katika ngazi ya kata zilenge maeneo yenye kasi kubwa ya maambukizo.
n Kujenga uwezo wa Kamati za Kudhibiti Ukimwi za Vijiji na za Kata ili kupambana na janga katika ngazi ya chini.
n Waratibu wa UKIMWI wa Halmashauri za Wilaya ambao pia ni maafisa maendeleo wa wilaya wana kazi nyingi sana. Ili kuweza kufanya kazi zao kwa ufanisi zaidi inabidi wafanye kazi za kuratibu shughuli za UKIMWI na si nyinginezo za ziada..
n Kuna haja ya waratibu wa UKIMWI wa Halmashauri za Wilaya kuwashauri Kamati za kudhibiti UKIMWI katika Mamlaka za Serikali za Mtaa jinsi ya kugawa pesa kwa usawa kwa asasi za kiraia zinazostahili kupewa pesa hizo kwa ajili ya kugharamia shughuli zao za kupambana na janga la UKIMWI. Kama kuna asasi isiyo ya kiserikali inayopata pesa kutoka sehemu moja, basi asasi isiyo ya kiserikali isiyokuwa na msaada ipewe kipaumbele.
n Katika miradi inayofadhiliwa, ufadhili unapokwisha, inabidi itengenezewe ufadhili mbadala ili iwe endelevu.
n Imependekezwa kuwa, kwa vile kuna utajiri wa ujuzi katika shughuli za Virusi vya UKIMWI/UKIMWI katika ngazi ya jamii ambazo haziwekewi kumbukumbu kwa hiyo kuna haja ya kuendeleza utamaduni wa kuweka kumbukumbu za ujuzi huu, na siyo kusubiri hadi wageni kutoka nje waje na kuweka, kuhifadhi na kumiliki kumbukumbu hizo.
n Watu wanaofanya kazi katika maeneo yenye kasi kubwa ya maambukizo ni kundi ambalo lipo katika hatari kubwa ya kupata maambukizo ya Virusi vya UKIMWI. Kwa hiyo, kwa vikunddi vilengwa kama wahudumu wa baa, wauzaji wa pombe za kienyeji, watumishi wa nyumba za kulala wageni na wasichana wanaohama kutoka baa moja hadi nyingine kutafuta wanaume, inabidi miradi maalum iendelezwe kuokoa kundi hili la walengwa, ambao wana tazamwa kuwa ni wafanyakazi wa biashara ya ngono.
n Kwa kuwa kuna uhaba wa vifaa vya ujelimishaji nchini inabidi kuwasiliana na watengenezaji wa vifaa hivyo kuhusu uwezekano wa kutengeneza vifaa vingi zaidi na kuviuza kwa taasisi zingine - inabidi itengenezwe ili kujua nini kilichopo na wapi vifaa vinapatikana na habari hizi kusambazwa kwa taasisi mbalimbali. Taasisi zinaweza kuombwa ziagize mapema ili zitengenezwe sambamba na mahitaji.
n Wahudumu wa baa waunde vikundi ili kujenga umoja na mshikamano baina yao katika kuendeleza mapambano dhidi ya UKIMWI.
n Utoaji wa elimu kuhusu matumizi ya kondomu kwa viongozi wa dini
n Kuimarisha na kuendeleza shughuli za kupambana na virusi vya Ukimwi na/au UKIMWI ambazo ni mifano bora.
n Kuendelea na uandaaji wa kinga.
n Kuendelea na kuorodhesha na kubaini asasi zote za kiraia na kata ili kutekeleza Mpango wa Jamii wa Pamoja.
n Imarisha uelimishaji rika kwa sababu zimethibitisha kuwa zinapunguza kasi ya maambukizo ya UKIMWI na magonjwa ya zinaa.
n Ongeza elimu rika katika maeneo yenye kasi kubwa ya maambukizo, shule za msingi na sehemu za kazi, ikiwemo sekta ya afya.
n Imarisha ukusanyaji wa habari hasa zinazohusu wagonjwa wa UKIMWI.
n Kupata mwitikio mkubwa zaidi kutoka kwa jamii sambamba na uongozi bora kutoka serikalini pamoja na asasi za kiraia kwa kupitia Kamati za Kudhibiti UKIMWI katika Serikali za Mitaa.
n Kuhamasisha jamii kuhusu dawa za kuongeza kinga ya mwili kwa kutumia washika dau.
n Kuwa na wafanyakazi wa afya wengi zaidi na wenye mafunzo kuhusu tiba za kuongeza kinga ya mwili.
n Kuendeleza miradi inayovuka mipaka kwa kushirikiana na nchi jirani (Malawi, Zambia na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo). Kama ilivyoonekana, kuna mchanganyiko na msongamano mkubwa wa watu kutoka Malawi, Zambia, na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo katika vitongoji vya mipakani, na imeelezwa kuwa ni kichochea kikuu cha janga la UKIMWI katika mkoa.
n Kusambaza habari na elimu na kufikia na kugusa, TACAIDS na washika dau wengine inabidi waendelee kuweka kumbukumbu na kuhadithia kuhusu mafundisho yaliyopatikana kutokana na shughuli za kupambana na Virusi vya UKIMWI na UKIMWI.
HITIMISHO
Kwa vile bado tuna idadi kubwa ya watu walio huru na maambukizo ya Virusi vya UKIMWI/UKIMWI, uzuiaji wa maambukizo unabidi upewe kipaumbele kama nguzo ya kwanza. Kila mtu awezeshwe kupitia elimu ili kufanya maamuzi ya kisomi kuhusu tabia zao kwani wengi hufanya vitendo kwa sababu ya kutokujua. Hata hivyo, dawa za kuongeza kinga ya mwili kama msaada wa ziada, isiyochukua nafasi ya uzuiaji wa maambukizo,
1. Taarifa ya Ziara ya Mkoa wa Mbeya
Tume ya kudhibiti UKIMWI Tanzania, Septemba 2007.
2. Takwimmu za Ofissi ya DPLO – Halmasshauri ya wilaya ya Mbeya, 2003
3. MMatokeo ya sensa ya watu ya 2002 ya Ofisi ya Mipango – Halmashauri ya wilaya ya Mbeya.
4. Taarifa ya VVU/UKIMWI na Magonjwa ya zinaa ya Mkoa wa Mbeya - Dr. J. Sewangi, Juni 2007
MSAMIATI WA KIUFUNDI
Bila Dalili – Isiyoonyesha dalili za ugonjwa ingawa maambukizo ya
ugonjwa yapo
Bakteria – Vijidudu, baadhi vina msaada kwa shughuli za mwili, lakini vingi
husababisha magonjwa.
Chembedamu nyeupe – Sehemu ya damu inayolinda mwili usivamiwe na kuingiliwa na vijidudu vyenye kusababisha magonjwa.
Dawa ya kutuliza – Dawa wanazopewa watu wenye matatizo ya kupata usingizi
Dalili – Maumivu na matatizo mengine yanayoelezwa na mgonjwa kwa
tabibu
Huzuni – Tatizo la kisaikolojia linalotokana na hisia za huzuni kubwa na
kupoteza matumaini.
Iliounganishwa – Katika mantiki hii, kuunganisha huduma za kuzuia/kutibu magonjwa ya zinaa na huduma za uzazi wa mpango na matunzo ya afya ya mama na mtoto.
Kusubiri – Kuachana na ngono kabisa.
Kuungua – Hali inayounganisha uchovu mkali pamoja na msongo mkubwa
wa kihisia
Kondomu – Kifuniko cha mpira kinachovaliwa na uume uliosimama wakati
wa tendo la ngono ili kuzuia mimba na kuambukizana na magonjwa ya zinaa .
Kuambukiza – kuweka au kuingiza vitu vyenye athari mbaya, kama vile
vijidudu vyenye kusababisha magonjwa.
Kuondoa maambukizo – Kuondoa au kutekeleza vitu vyenye athari mbaya, kama vile vijidudu vyenye kusababisha magonjwa.
Kupeleka – Kumpeleka mgonjwa kutoka nyumbani au kwenye jamii kwenda
kwenye kituo cha afya au kutoka kwenye kituo cha afya kwenda kwenye jamii au nyumbani.
kwa watu waishio na Virusi vya KIMWI/UKIMWI zinalenga zaidi kwenye usafi wa mwili, lishe, tabia za ngono, misaada, tiba ya hali zinazohusiana na UKIMWI na tiba za mazoezi ya mwili
Mfumo wa Kinga – Sehemu ya mwili inayopambana na maambukizo ya magonjwa.
Maambukizo – Uvamizi na uzaliaji katika mwili wa vijidudu vyenye kusababisha magonjwa.
Moduli – Katika mantiki hii, sehemu ya utaratibu wa mafunzo.
Magonjwa ya zinaa – Kundi la magonjwa ya wanawake na wanaume
yanayoambukizwa kwa kupitia kufanya tendo la ngono.
Maagizo ya daktari – Maelezo ya maandishi ya tabibu yanayotambulisha jina la dawa zinazotakiwa kutumiwa na mgonjwa, na jinsi ya kuzitumia.
Mnyonyeshaji mbadala – Mwanamke anayemnyonyesha mtoto wa wanamke mwingine
kama mwanamke mwenye mtoto atashindwa kufanya hivyo mwenyewe
Shauku – Tatizo la kisaikolojia linalosababisha hisia za wasiwasi na woga
Shahawa – Majimaji yenye mbegu za uzazi zinazotengenezwa na
mwanaume wakati wa ngono
Tathmini ya rika – Tathmini na maelezo kuhusu elimu au uwezo wa kazi wa mfanyakazi mwenza
Ushauri Nasaha – Mawasiliano kati ya watu wawili ambapo mmoja ana
tatizo na mwingine anajaribu kusaidia kulifafanua.
Uchunguzi /Yakini – Maelezo ya tabibu kuhusu mtu ananaumwa ugonjwa gani
Utoaji wa dawa – Jinsi dawa zinavyogawiwa kwa mgonjwa
Usafi wa mazingira – Kuweka mazingira, nyumba, kiwanja nk katika hali ya usafi
Usafi wa Mwili – Kuweka mwili na mazingira katika hali ya usafi.
Uaminifu – Kufanya tendo la ngono na mtu mmoja tu, ambaye naye hafanyi
tendo la ngono na mtu yeyote isipokuwa wewe.
UKIMWI – Upungufu wa kinga Mwilini, ugonjwa unaopunguza uwezo
wa mwili kujikinga na magonjwa, inayosababishwa na kuambukizwa virusi vya UKIMWI.
Virusi – Vijidudu vinavyosababisha magonjwa
FOLLOW UP AND ASSESSMENT
REPORT ON HIV AND AIDS
MBEYA REGION
TANZANIA COMMISSION FOR AIDS (TACAIDS)
TABLE OF CONTENTS
Page No. List of Abbreviations... ii Introduction... ... iv Acknowledgement... vii Chapter 1:Observations and Findings... 1 Chapter 2: Challenges... 22 Chapter 3: Achievements... 24 Chapter 4: Recommendations... 29 Conclusion... 31 Reference... 31 Glossary... 32
ACCA AIDS Control in Companies in Africa AIDS Acquired Immune Deficiency Syndrome ANC Ante Natal Clinic
ART Anti Retroviral
BACAIDS BAKWATA Commission for AIDS
BAKWATA Baraza Kuu la Waislamu Tanzania/ National Muslim Council CARF Community AIDS Response Fund
CBO Community Based Organization CHAC Council HIV and AIDS Coordinators CHMT Council Health Management Team CMAC Council Multi Sectoral AIDS Committees CODES Cohort Development Study
COPTA Community Planning Tools for AIDS Intervention CPP Community Partnership Plan
CSO Civil Society Organization
DACC District AIDS Control Coordinator DAS District Administrative Secretary
DC District Commissioner
DED District Executive Director
DFID Department for International Development DMO District Medical Officer
DRC Democratic Republic of Congo
EU European Union
FBO Faith Based Organization GTZ German Technical Assistance
HBC Home Based Care
HIV Human Immunodeficiency Virus HLM Health Learning Materials HSIS HIV Super Infection Study HTA High Transmission Area
IEC Information Education and Communication JICA Japanese International Cooperation Agency LGA Local Government Authority
MARVAD Mbeya Anti Retroviral Initiation Study
MSD Medical Stores Department MTEF Mid-Term Expenditure Framework
NACOPHA National Council of People Living with HIV/AIDS NACP National AIDS Control Programme
NGO Non Governmental Organisation OVC Orphans and Vulnerable Children PE Peer Educator/ Education
PEP Post Exposure Prophylaxis PLHA People Living with HIV/AIDS PLHIV People Living with HIV
PLPWHA People Living Positively with HIV/AIDS PMTCT Prevention of Mother to Child Transmission PSI Population Services International
RACC Regional AIDS Control Coordinator RAS Regional Administrative Secretary RC Regional Commissioner
REO Regional Education Officer RFA Regional Facilitating Agency RMO Regional Medical Officer RS Regional Secretariat
SPW Students Partnership Worldwide STD Sexually Transmitted Diseases STI Sexually Transmitted Infections TAC Technical AIDS Committee TACAIDS Tanzania Commission for AIDS TAZARA Tanzania Zambia Railways Authority
TB Tuberculosis
TCCIA Tanzania Chamber of Commerce, Industry and Agriculture TGPSH Tanzania German Programme to Support Health
TMAP Tanzania Multi-Sectoral AIDS Project TOT Training of Trainers
Mbeya Region covers a surface area of 64,000 square kilometers and has a population of 2,070,046 (990,825 men and 1,079,221 women). The child bearing age (15-49 years) population is 423,945. The HIV prevalence rate of Mbeya is 13.5%, the highest in the country (the national HIV prevalence rate is 7 %). Mbeya has a good communication network as highways cross the region connecting the harbors of Dar es Salaam and Mombasa with Zambia and Malawi together with other African countries through road and railways creating a corridor of social interaction between the three countries and other in the South.
The main objective of the Mbeya Mission Team was to conduct a monitoring and evaluation of the HIV/AIDS situation in Mbeya region. This was a routine mission of TACAIDS to visit the region for a better understanding of the interventions related to HIV/AIDS in the region. The timetable was very comprehensive and designed for the team to meet different groups of people including faith based organizations, girls and boys, women, people living with HIV/AIDS, specific target groups such as barmaids and government sectors like education, agriculture and community development. Today HIV/AIDS is recognized not only as a major public health concern, but also a social and development problem in the country, region, district and community at large. While in Mbeya region the team visited four districts out of eight in the region. The districts visited were selected by regional authorities in consultation with the district authorities.
TACAIDS had prepared questionnaire forms that were distributed to various groups before visiting these respective groups for discussions. The TACAIDS team was divided into teams which visited different groups such as women, young people, people living with HIV/AIDS, elderly people, bar workers and guest house attendants, faith based institutions, educational institutions, CTC, research centers and key selected RFA organizations.
The team visited the districts of Kyela, Chunya, Mbarali and Mbozi. In these districts the visiting schedule was planned by CHAC and several groups including NGOs and government officials such as district heads of the departments of agriculture, education and administration. Heads of primary schools, ward counselors and faith based organizations such as BAKWATA were also involved in the deliberations.
The methodology used was participatory whereby all groups were involved during discussion. The aim of the discussion was to enlighten the TACAIDS mission on the
The consultation meetings helped TACAIDS to have an advantage by creating awareness, advocating and sensitizing the community groups to understand that the war against HIV/AIDS is for them and not for anyone else. Such kinds of motives motivate the stakeholders at regional and district level to keep on fighting this scourge disease.
The advantages of this methodology was also to provide technical support on fund raising modalities and technical issues such as funding procedures and proper settlement of funds where it was identified during the discussion that to some recipients there was a problem especially in knowledge of the procedures.
ASSESSMENT TEAM
The Mbeya Mission Report was prepared by TACAIDS, which sent a team to Mbeya to conduct a monitoring and evaluation of the HIV/AIDS situation in Mbeya region. The team comprised of TACAIDS staff, NACOPHA representatives, Ministry of Health and Social Welfare staff, Regional and District Health authorities, Council HIV and AIDS coordinators, GTZ (the Regional Facilitating Agency) staff, development partners from the World Bank and journalists.
TACAIDS
Hon. Lediana Mng’ong’o, MP, Commissioner Dr. Fatma H. Mrisho, Executive Chairperson Mr. Sam Komba, Legal Officer
Mr. Charles Kamugisha, Department of District and Community Response Mr. Chaddy Anthony, Department of Policy and Planning
Mr. Simon Keraryo, Department of Advocacy and Information
Mr. Shedrack Mpabangaya, Department of Finance and Administration Mrs. Hulda Tairo-Urasa, Department of Finance and Administration
Council HIV and AIDS Coordinators (CHACs)
Mr. Hebel A.Luvanda Mr. A.R. Chavula Ms. Rachel Mbelwa
Regional Facilitating Agency
Dr. Bruno Masumbuko, Team Leader Frida Radegunda Godfrey
Upendo Chabili
Development Partners
Ms. Angelica Schrettenbrunner, GTZ AIDS Program Coordinator Mr. Yunus Koshuma, GTZ
Dr.Emmanuel Malangalila, World Bank (participated on the first day)
Journalists
Mr. Benny Mwaipaja, ITV
Mr. Festo Sikagonamo, ITV (Camera) Mr. Niko Mwaibale, TVT
Mr. Ngujuna Kalanja, TVT (Camera)
Drivers
Gabriel Chonya Barick Dawa Danstan Kapinga Habib Nzomukonda
ACKNOWLEDGEMENT
Acknowledgements are extended to the following individuals for their invaluable support and assistance in the making of this report : youth, women, people living with HIV/AIDS, elderly people, bar workers, guest house attendants, faith based institutions such as BAKWATA (the National Muslim Council of Tanzania), educational institutions such as primary and secondary schools, research centers, key RFA selected organizations, ward counselors and district department heads of agriculture, education and administration of Kyela, Chunya, Mbarali and Mbozi districts.
Fatma Mrisho Executive Chairman
CHAPTER ONE
OBSERVATIONS AND FINDINGS
1. Stakeholders and target groups
1.1 Youth groups
The participation of young people was active and effective in the discussion during the monitoring visit. They explicitly mentioned that the rapid increase in population, rural to urban migration, frequent and excessive use of alcohol, problems in the family, poverty – low income, unemployment among youth, indecent provocative dressing, peer pressure to have luxury commodities, and easy access to pornography via TV, videos and Internet are among the drivers of the epidemic. It was also noted that students are at risk on the way to school and at their rental houses and hostels without parental guidance and control.
A number of youth groups are active in disseminating HIV prevention information through various means e.g. theatre, drama and comedy, but reported being restrained by shortage of financial resources specifically transport to scale up their innovative activities and programmes. They also noted not having enough and correct information on HIV/AIDS and life skills. Capacity building is highly needed in these identified areas as well as an increase in support for youth groups.
1.2 Women
Observations:
n Sexually arousing dressing - “Vimini” , “KK” and “Vitop” n Women are very active in business and very mobile n There is lack of notification of HIV status to a partner
tend to become careless.
n Some of them had no other source of income and had no other choice than working in bars. They expressed the need for making female condoms more available.
n Some bar girls mentioned receiving a basic monthly salary of about 15,000 Tshs. They were not allowed to negotiate higher pay with the client but were allowed to take gifts.
1.3 The Disabled:
Inadequate knowledge of HIV transmission was noted amongst the group of disabled people. They said that they did not see sense in going for HIV test because they don’t see sense in the advice generally given to PLHAS to improve their diet because of their poverty. This group said that no or inadequate interventions are being directed to them whereas men do approach disabled girls under the belief that they are not infected with the virus. And because of their poverty men prefer sex with disabled girls in exchange for services rendered to them. They expressed concern for the society to recognize their rights , sensitize and educate them on skills regarding HIV transmission so that the educated few could in turn impart such knowledge to their fellows.
1.4 Orphans and Vulnerable Children
It was observed that there has been an increased number of OVC in the community. Each district has NGOs supporting orphans and vulnerable children, e.g. in Kyela there is the NGO Oaktree which is supporting orphans and vulnerable children through material aid such as school uniforms, books, school fees, vocational training, income-generating activities and medical treatment. The scope is however limited with a relatively small number of beneficiaries. Other NGOs supporting OVCs in Kyela are St. John Hus. Centre and USACA, which cares for 521 orphans.
The following are some planned activities in the region: n To provide health service to 192 OVC groups [CHF fee.]
n To identify OVC in 17 Wards. 4370 OVC are identified, female 2622 and male 1748. among them 1710 are under 5 years
n To co-ordinate the distribution of school materials to 524 OVC. 1.5 The Roman Catholic Church in Mbeya:
The church has a priest appointed as HIV/AIDS coordinator and he coordinates all HIV activities in 30 parishes within the diocese. Current interventions include: VCT, HBC and ARV services carried out by their mission hospitals and health workers. The church mobilizes youth and adult groups through their networks and cares for 47 orphans. They also entertain awareness programmes in schools and have put HIV on the agenda during preaching. The Roman Catholic Church is silent on the use of condoms. They are neither