• Tidak ada hasil yang ditemukan

5.2 Fani ya Tondozi Wakati wa Ukoloni

5.2.1 Utungaji wa Tondozi

5.2.1.1 Utungaji wa Papo kwa Papo

Milman Parry (1928-1930) na mwanafunzi wake Albert Lord (1981), wameelezea utungaji wa papo kwa papo wa kazi za fasihi simulizi. Parry alianza kujiuliza ni kwa vipi tendi za Homer zilitungwa, je, zilikuwa simulizi au andishi? Parry alifanya uchunguzi katika jamii za Wayugoslavia ingawa uthibitisho wa dai hili ulikuwa haujatolewa. Samwel (2011) anasema Parry alianza kwa kuchunguza mishororo 25 ya mwanzo ya Iliad na Ulisei (odyssey) ili kuona ni kwa kiasi gani tungo hizo mbili ni za kifomula. Matokeo ya utafiti wake yalimshangaza. Aligundua kuwa takribani 70% ya mistari 27,000 katika tendi hizo ilikuwa ya kifomula, kutokana na hilo Parry akahitimisha kwamba tungo hizo ni nudhumu, ni simulizi (si andishi) na, niza kimapokeo.

Miaka michache baadaye baada ya kifo cha Parry miaka ya 1935, Lord aliundeleza utafiti wake na kutoa mchango wenye manufaa. Aliongezea kipengele cha “formulaic expression” kauli ya kifomula, katika nadharia ya fomula simulizi.

Alisema wakati mwingine hutokea watendi kutumia fomula bila kuzibadilisha, wakati mwingine, huweza kubuni na kutumia kauli zenye muundo wa fomula. Alielezea kauli za kifomula kuwa ni mshororo au kipande chenye umbile la fomula.

Mchango mahsusi wa Lord ni kwenye kipengele alichokiita “theme” na baadaye

kipengele hicho kikaitwa topo kwa Kiswahili. kwa maelezo ya Lord, theme ni kipengele kinachorudiwa rudiwa “repeated incidents and descriptive passages”. Tofauti na fomula, topo hailazimiki kufuata urari wa mizani au kujirudiarudia kwa neno, bali huwa na umbo zalishi lenye kubadilika kulingana na mazingira ya usimulizi. Kwa maelezo haya topo hutegemea sana muktadha na utendekaji wa tukio.

Topo humsaidia fanani kuijenga na kuisimulia kazi yake kwa haraka wakati wa utendaji, maana topo tayari zimo katika jadi na akili yake, anachohitaji ni kuziainisha, kuzirekebisha kidogo kulingana na mahitaji.

Wataalamu mbalimbali kama vile Jahn (1961) na (1968), Okpewho (1979) na Mulokozi (2002), walijaribu kuirekebisha kulingana mitazamo yao. Kwa maelezo ya Mulokozi (2002) akizungumzia enanga anasema maelezo ya fomula yaanzie katika ngazi ya maana. Fomula kama inavyotumika katika tendi za enanga ni wazo- kiini radidi la kidhahania na kimapokeo. Hivyo basi fomula hubainishwa kwetu kupitia sura mbalimbali wakati wa uwasilishaji. Maumbo hayo ameyaita alomofu (alloforma-Mulla). Dhana hii ya fomula kwa mujibu wa Mulokozi, ndiyo inayotumika katika utafiti huu inaboresha ufafanuzi wa awali wa akina Lord na Parry. Aidha Mulokozi anapendekeza dhana ya “Theme” iliyopendekezwa na Lord

na Parry, ambayo tayari inatumika kumaanisha dhamira/wazo kuu. Theme katika nadharia ya fomula simulizi iitwe topo. Mulokozi (2002: 132-135) anaifasili topo kwa kusema:

A traditional or Conventional stock incident or description which regularly reformulated in different stories and context by the oral bards to build up Oral narrative poems during performance.

Kitushi au sawiri ya kikaida ya kijadi ambayo husimuliwa na watendi simulizi wakati wa hadithi na miktadha mbalimbali ili kutunga tungo simulizi wakati wa utendaji.

Kwa jumla, msimamo wa Parry, Lord na wafuasi wao ni kwamba fomula na topo hazihusishi kukariri. Hii ina maana kazi za fasihi simulizi, zikiwamo tondozi, hutungwa papo kwa papo wakati wa utendaji wake. Huu ndiyo ukawa msingi unaotumiwa na wanafasihi kuwa tondozi zilikuwa zinatungwa papo kwa papo.

Kuna wakati wasanii hukatokea wakaenda mahali fulani ambapo wanatakiwa kughani au kuimba na muhusika hajawahi kumuona, wanapomuona tu kwa mara ya kwanza wanatunga papo hapo. Katika utafiti huu kati ya wasanii kumi ambao mtafiti alihojiana nao alipowauliza kuhusu utungaji wa tondozi wote kwa nyakati tofauti walijibu kuwa, wao huwa wanatunga kulingana na muktadha husika unawataka wao wafanye nini kwa wakati huo. Utungaji huu ulidhihirishwa wakati mtafiti alipokuwa akihojiana nao, baadhi yao waliweza kutunga tondozi kadhaa zilizomhusu mtafiti kwa nyakati tofauti. Wanachofanya ni kuuliza utokako, ukoo wako na majina yako baada ya hapo mengine yote wanayafanya wao kama wasanii. Mfano msanii Adamson kutoka kijiji cha Selya alimuuliza mtafiti majina yake na asili yake kisha akatunga tondozi hii papo hapo wakati wa mahojiano.

Jedwali Na. 5.1:Tondozi Inayohusu Watoto Yatima

Na Kinyakyusa Kiswahili

1. Mhh, ahaa Rose, itenga, kalapa, Itundu lya ng’ombe

Mmh, ahaa Rose, Itenga, Kalapa, Itundu lya ng’ombe

2. Linga gwisile kukajha kwa Selya, atukuponyagha twe bhana bha bhalondo Rose

Siku ukija nyumbani kwetu Selya tutakusalimia sisi watoto wa maskini Rose

3. Gwe gwa kubhusokelo, kwa Mwakaleli, kunjuni inyanga, kulisu ilyonywa, kuno bhafumile abhimbi bha kwanda Rose

Wewe wa Busokelo, Mwakaleli, kwenye ndege wazuri, majani mororo, kule walikotokea wasomi wa mwanzo Rose

4. Kusekondari jha Mwakaleli, kumaendeleo Rose

Kwenye sekondari ya Mwakaleli kwenye maendeleo Rose

5. Linga twaghanile munjila

gumbonyeghe, ne Mwamulangala, ne Kilembe, ne Mwailamula

Tukikutana njiani uwe unanisalimia, mimi ni Mwamulangala, mimi Kilembe, Mimi Mwailamula

6. Ngundendesyege pakumbonya, kangi ngaja ni lyojo, ngamanya ukujwegha na bhandu

Uwe unanibembeleza unaponisalimia, tena mimi sina hasira, sijui kupigizana kelele na watu

7. Gundendesyeghe bho ulu gwalindendesisye bho kumbapa

Unibembelezage kama vile

Rose Rose 8. Gwakolile indumbula mmabhoko,

undumegho alinkuti pamo unkasi gwangu ikufwa

Ulishika roho mkononi, mumeo alifikiri labda mke wangu atakufa

9. Po apa ngubhule unkasi gwangu jho kalebhela Ngondo, Musyani, Kifulagha, gwa mu Mbhighili

Ngoja nikuambie, mke wangu majina yake ni Kalebela, Ngondo, Musyani, Kifulanga mtoto wa Mbigili

10. Unkasi gwangu umpimba, untitu, imbaghi ngati kifigho kya ikanisa, mwe bhaputi mweee

Mke wangu mfupi mweusi na mwanya kama mlango wa kanisa, jamani

wachungaji mweee 11. Linga nfwile unkasi gwangu ise

akonyole ilisu, ambyagisye kumbulo

Nikija kufa mke wangu atakata jani na kunipangusa puani

12. Papo linga tufwile tukunyalisya, tukufwana mbwa jifwilile pa lami inditu

Kwasababu tukifa tunachefua, tunakuwa utafikiri mbwa aliyefia kwenye lami nyeusi.

13. Aikumbyagisya kumaso aikuti ufwile naloli Mwambapa, ufwile naloli Mwamulangala

Atanifuta usoni atasema, ni kweli umekufa Mwambapa, umekufa kweli Mwamulangala

14. Aikundwala kukajha, kwa Kasenga, kwa Mwaihojo, kwa Kaponela

Atanipeleka nyumbani kwa Kasenga, kwa Mwaihojo, kwa Kaponela

15. Aikukolela, ise ime pakyamba kya malajha, ikundwala unkasi

gwangu umpimba untitu

Atakuja kuita, atakuwa amesimama kwenye mlima Malaya, wakati

ananipeleka mke wangu mfupi mweusi 16. Umama gwangu ugwa kighili,

ugwa misimu, unganga gwa jadi amunkolelege kanunu mutunze ifyombo, isa kughomoka kunyuma nyuma

Mama yangu mwenye kichaa, mwenye nguvu za mizimu, mganga wa jadi, mtamshika vizuri mutunze na vyombo vyake atakuja atembee kwa kurudi nyuma nyuma

17. Bho ikuti findu fiki muti abhinile tukuntwala Kwitete kusipitali

Atakaposema ni kitu gani hicho, muje mumwambie anaumwa tunaenda naye hospitali ya Itete

18. Unkasi gwangu Kalebela Musyani Ngondo gwa Mumbighili

Mke wangu Kalebela Musyani, Ngondo wa Mbigili

19. Aikwima pakyamba kya Malaja bho bikuti fiki bhati

Atasimama kwenye mlima Malaya, watakapomuuliza ni nini tena 20. Aikuti ingongobhe jhangu jifwile

ulufwa, ingongobhe jha Mwaihojo jifwile ulfwa

Atasema jogoo wangu amekufa kideli, jogoo wa Mwaihojo amekufa sababu ya kideli

21. Bhati jifwile ingongobhe ijhi jhali kwa Mwandobo, kwa Kaponela,

Eti imekufa ngo’mbe yangu iliyokuwa kwa Mwandobo, kwa Kaponela, Kwa

kwa Mwakatumbula, Kwa Mwakilili, kwa Mwaisumo

Mwakatumbula, kwa Mwakilili, kwa Mwaisumo

22. Unkasi gwangu bho ikulila ikupikanika x 2

Mke wangu wakati analia kwa uchungu akijipigapiga

23. Kangi abhalumbu bhitu bhikulila bhikupikanika

Tena dada zetu wanalia na kujipiga piga

24. Aghunkolele umwanako, Tupilike Uje umwite binti yako Tupilike 25. Tupilike unka Mwamulenga, unka

Mwakitwange, unka Mwaihojo, unka Mwakasula, unka Mwakilili

Tupilike mke wa Mwamulenga, mke wa Mwaitege, Mwakasula, mke wa

Mwakilili 26. Auti ingongobhe jha Banyandobo

jifwile

Utasema jogoo wa watu wa Ndobo amekufa

27. Kangi jifiwile ulufwa ejhoo Tena imekufa kideli

28. Rose ahaa x 2 chunga sana yatima Rose ahaa x 2 chunga sana yatima

Hivyo katika utafiti huu tumebaini kuwa pale ambapo kulikuwa na utungaji wa papo kwa papo wa tondozi mtunzi aliongozwa na fomula na topo ambayo tayari anazo anachokifanya ni kuongeza yale ambayo kwa wakati huo yamejitokeza kwa muktadha aliopo.