• Tidak ada hasil yang ditemukan

Kigezo cha Tabia na Matendo ya Mtu

4.4 Vigezo Vinavyotumika Kuteua Majina ya Asili katika Koo za Ginantuzu . 104

4.4.6 Kigezo cha Tabia na Matendo ya Mtu

Majina yanayotokana na tabia na matendo ya mtu kwa kawaida huakisi mienendo ya

wahusika. Mienendo hiyo hujumuisha ubishi, ukarimu, ukaidi, ufuska, majivuno,

usafi, hasira, upole, uchoyo, ukali, wema, ulevi ama ukorofi. Watafitiwa 7 ambao ni

sawa na asilimia 8.75 walibainisha kuwa tabia na matendo ya mtu ni mojawapo ya

Tabia na matendo hayo yalifanywa na waanzilishi wa koo husika katika jamii. Tabia

na matendo katika jamii yalitofautiana kati ya mtu mmoja na mwingine kama

anavyodai Adrey (1970) kwamba, kila mtu katika jamii ana tabia na matendo

yanayoweza kumtofautisha na wengine. Salapion (2011) naye katika utafiti wake

alishadidia haya kwa kusema kuwa, majina yanayotokana na tabia kimsingi huakisi

mienendo ya wahusika. Alitolea mifano michache ya majina katika jamii ya wahaya

ambayo yanatokana na tabia kama vile ‘Karikwera’ yaani mtu msafi asiye na doa na

‘Izooba’ yaani mtu mzuri na mwenye haiba. Hata katika koo za Ginantuzu kama ilivyoelezwa hapo mwanzo kuwa baadhi ya majina ya asili yanatokana na tabia na

matendo ya watu wa jamii hiyo. Utafiti umebaini kuwa katika koo za Ginantuzu, kuna

majina ya asili yenye maana yatokanayo na tabia na matendo ya watu. Tabia na

matendo ya wazazi ama ndugu wa karibu wa watoto hao ndizo zilizopelekea watoto

hao kuitwa majina hayo. Kwa mujibu wa watafitiwa waliofikiwa na mtafiti kwa njia

ya mahojiano na hojaji walieleza kuwa, tabia na matendo katika jamii yaliyopelekea

kupatikana kwa majina hayo mara nyingi yalikuwa yanaakisiwa kutoka kwa wazazi

wa watoto hao na si watoto wenyewe. Ingawa kwa kiasi kidogo yalifanywa na watoto

wenyewe lakini zaidi yalitoka kwa wazazi. Kwa mfano jina ‘Machilu’ au ‘Buchilu’ ni jina ambalo alipatiwa mtoto kutokana na tabia yake ya kupenda kulialia sana bila

sababu wakati wa utoto wake. Baadhi ya majina yanayotokana na tabia na matendo ya

mtu ni pamoja na Malaya, Kilekawanzile, Kuyela, Lusumbula, Masemba, Kabudi,

Mayombo, Kilila, Nhonge, Mnyumba, Mahela, Walwa, Kasabuku, Ngokolo, Maseko,

Nkali, Mkali, Buyegi, Nkwabi, Butogwa, Long’we na Mayuma. Hapa chini ni

ufafanuzi wa maadhi ya majina yaliyotokana na tabia na matendo ya watu

1. Ngokolo (mvivu) Hili ni jina ambalo alipatiwa mtoto wa kiume ambaye

mwanzilishi wa jina hilo alikuwa na tabia ya uvivu wa kufanya kazi.

Wazazi wa mtoto huyo waliamua kumpa mtoto wao jina hilo ili asije

akarithi tabia na matendo ya mwanzilishi wa jina hilo. Wakati

mwingine jina hilo lilitolewa kwa mtoto huyo kama kuweka

kumbukumbu ya mwanzilishi wa jina hilo lisije likapotea.

2. Kuyela (mtembezi) Jina hili hupewa mtoto wa kiume ambaye wazazi wake

aumwanzilishi wa jina hilo alikuwa na tabia ya utembezi kupita kiasi.

Tabia hii ya utembezi katika koo za Ginantuzu ilipigwa vita sana

kwani mtembezi daima katika jamii alionekana kutokuwa na kitu

chochote cha kiuchumi kwani muda wake mwingi aliiutumia

kutembea badala ya kufanya kazi inayozalisha mali. Hivyo jina hilo

lilitolewa kwa mtoto kama kukemea hali hiyo isijirudie tena kwa

mtoto aliyepewa jina hilo.

3. Masemba (vituko/utani) Hili ni jina alilopewa mtoto wa kiume na wazazi

wake ambaye alikuwa na vituko sana au mwazilishi wa jina hilo

alikuwa na vituko vingi vyenye kuchekesha katika maisha yake. Watu

wenye vituko katika jamii ya Ginantuzu kwa kiasi kikubwa

walipendwa sana na walitakiwa sana kuwepo katika shughuli yoyote

iliyokuwa inafanywa kwa jumuia. Hivyo mtoto aliweza kupewa jina

hili kama ukumbusho wa mwanzilishi huyo.

4. Mayombo (mwenye vurugu) Jina hili hupewa mtoto wa kiume ambaye wazazi

Kutokana na majibu wa watafitiwa walisema kuwa katika jamii yao

kama zilivyo jamii nyingine kulikuwapo na watu ambao walipenda

sana kufanya vurugu nje au ndani ya jamii yake. Watu kama hao

walipewa jina hilo kama ishara na utambulisho kwa jamii husika.

Hivyo ili kutunza kumbukumbu ya mtu huyo jina lake lisipotee katika

ukoo watoto wengine waliweza kupatiwa jina hilo kwa ajili ya

ukumbusho.

5. Kilila (kulia) Hili ni jina analopewa mtoto wa kiume ambaye alikuwa na tabia

ya kulialia bila sababu wakati wa utoto wake. Wakati mwingine jina

hili hupewa mtoto kama jina la ukoo ambapo mwanzilishi wake

alikuwa na tabia hiyo ya kulialia bila sababu ya msingi. Jina hili

wakati mwingine huitwa ‘Machilu’ likiwa na maana hiyo hiyo ya kulialia bila sababu ya msingi.

6. Mnyumba (nyumbani) Jina hili alipewa mtoto wa kiume ambaye mwanzilishi

wa jina hili alikuwa na tabia ya kukaa ndani ya chumba au nyumbani

kwake tu. Katika koo za Ginantuzu wanaume walikuwa wanatakiwa

kukaa nje wakati wote na sio ndani ya chumba au mwanaume

alitakiwa wakati mwingine atoke nje ya familia yake kwa ajili ya

kukutana na wanaume wenzake kwa kubadilishana mawazo. Hivyo

kwa mwanaume ambaye hakuwa na tabia hizo alipewa jina hilo ili

kusadifu tabia na matendo aliyo nayo kwa jamii husika.

7. Walwa (pombe) Hili ni jina analopewa mtoto wa kiume jina ambalo

kiasi kwamba alikuwa hawezi kukosekana mahali palipo na pombe.

Wakati wowote mtu huyo anapohitajika na jamii, mahali pa

kumtafutia ilikuwa ni vilabuni. Watu wengine wenye tabia na

matendo kama haya walipewa jina la ‘Mahela’ likiwa na maana ya machicha ya pombe ya kienyeji. Watu hawa wakati mwingine

walikuwa mafundi wa kutenganisha pombe na machicha ya pombe

hivyo ikapelekea kupatiwa jina hilo la Mahela.

8. Nkwabi (mtafutaji mali) Jina hili alipewa mtoto wa kiume akirithi kutoka kwa

wazazi/ waanzilishi. Mwanzilishi wa jina hili alipewa kutoka na tabia

ya utafutaji mali kwa njia halali. Katika jamii ya Ginantuzu mtu kama

huyu alipendwa na kila mtu mwenye moyo wa utafutaji mali.

Utafutaji mali ulikuwa ni msingi wa maisha katika koo za Ginantuzu

hivyo jina kama hili lilipendwa na jamii na linapatikana kwa wingi

katika koo za Ginantuzu mpaka sasa.

9. Mkali (ukali) Hili ni jina analopewa mtoto wa kiume jina ambalo limetokana

na mzazi au mwanzilishi wa jina hilo kuwa na tabia ya ukali wakati

mwingi. Tabia kama hii haikukubalika katika koo za Ginantuzu. Mtu

aliyeonekana kuwa na tabia hiyo ya ukali bila ya kuwa na sababu za

msingi aliweza kupewa jina hilo kama kusadifu tabia aliyonayo.

10. Mayumila (kutoa kitu bila kipimo maalum) Jina hili lilitolewa kwa mtoto wa

kiume akirithi kutoka kwa mwanzilishi aliyekuwa na tabia nzuri

iliyokubalika kwa jamii kiasi kwamba alikuwa anatoa kitu chochote

ilikuwa inamilikiwa na wachache sana. Wachache hawa walipewa

jina hili kama zawadi ya kusadifu tabia na matendo waliyo nayo.

Watu wengingi jina hili lilifupishwa na kuitwa ‘Mayuma’.

Kutokana na ufafanuzi wa majina hayo hapa juu, utafiti umebaini kuwa tabia na

matendo ya mtu ni kigezo kilichotumiwa na koo za Ginantuzu kutolea majina katika

jamii yao na majina hayo huwa na maana tu kwa jamii ya Ginantuzu. Mtoto

anayepewa jina la aina hiyo kutambuliwa kuwa yeye ni Mnyantuzu kutokana na jina

la Ginantuzu linalomtambulisha kwa jamii yake. Katika sehemu hii, kupatikana kwa

majina haya kwa kutumia kigezo cha tabia na matendo ya mtu aliyonayo katika jamii

anamoishi kunatimiza moja ya lengo mahususi la utafiti huu lililolenga kuonesha

vigezo vinavyotumika katika kuteua majina ya asili katika koo za Ginantunzu. Aidha,

kupatikana kwa data hizi kunadhihirisha kufaa kwa nadharia ya uumbaji ambayo

imetumiwa na mtafiti kama mwongozo wakati wa kukusanya na kuchambua data za

utafiti huu.