• Tidak ada hasil yang ditemukan

Muktadha wa Kudokeza Udunishaji

4.5 Miktadha ya Majina ya Asili katika Koo za Ginantuzu

4.5.4 Muktadha wa Kudokeza Udunishaji

Udunishaji ni hali ya kukifanya kitu kuwa na thamani ndogo yaani kukiteremsha kitu

unaotumika kuelezea majina ya asili katika koo za Ginantuzu. Jedwali namba 4.28

linaonesha uwepo wa majina ya asili yanayodokeza muktadha wa udunishaji.

Watafitiwa kupitia njia ya hojaji na mahojiano walisema kuwa, katika koo za

Ginantuzu yapo majina ambayo walipewa baadhi ya watu kwa kudokeza muktadha

wa udunishaji. Baadhi ya majina hayo ni pamoja na Budulungu, Ndalahwa, Shunula,

Buga, Butule, Ntengo, Ding’ho, Galedi, Golomanda, Holohondo. Bukela, Ng’holo, Shagembe, ng’olo, Sagala, Ng'oba, Nhungo, Ngokolo na Mnyumba. Watafitiwa waliendelea kusema kuwa jamii katika koo za Ginantuzu ziliweza kuwadunisha

wahusika wa majina hayo kwa kuwapa majina ya vitu ambavyo havikuwa na thamani

kwao. Lengo la kuwapa majina hayo ilikuwa kuwafanya wahusika wa majina hayo

wasiwe na tabia na matendo ya majina ya vitu hivyo ambavyo havikukubalika katika

jamii. Miongoni mwa baadhi ya majina yaliyotajwa, majina yaliyoonekana kutumika

zaidi katika koo za Ginantuzu ni pamoja na Budulungu, Nhungo, Bukela, Galedi,

Shunula, Ntengo, Holohondo, Golomanda/Goma, Ng’holo/Makolo, Shagembe, ng’olo, Ng'oba, Ngokolo na Mnyumba. Ufafanuzi wa baaadhi ya majina haya ni kama ifuatavyo:

1. Budulungu (ng’ombe) Maana halisi ya jina hili ni ng’ombe mkubwa ambaye

hakuwa na afya nzuri katika kundi la ngombe wengi tangu akiwa ndama.

Jina hili lilitolewa kwa mtoto wa kiume akirithi kutoka kwa mwanzilishi

kwa kuashiria afya yake kutoridhisha katika ukoo au jamii yake kwa

ujumla. Lengo la kupewa jina hili ni kwa ajili ya kuondokana na tatizo

hilo linalomkabili. Jina hilo linaweza kuwa la kuitwa, kutaniwa au kujiita

mwenyewe. Ingawa imani ya jamii katika koo za Ginantuzu ni kuwa jina

kumkinga asipatwe na hali ambayo hawaihitaji kwani mwenye jina

akuapo hufanya juu chini asisadifu jina husika. Kwa kufanya hivyo

watakuwa wamemwokoa kwa njia moja au nyingine mhusika wa jina hilo.

2. Nhungo (mnyama) Maana halisi ya jina ni mnyama pori jamii ya mbwa. Tabia

ya mnyama huyu huwa anajisaidia haja kubwa sehemu moja tu kwa

mwaka mzima na anausingizi sana wakati wa mchana na ni msahaurifu

kweli na kumbukumbu kidogo. Mnyama huyo hata akiwa mbali hukata

majani na kuziba sehemu ya haja kubwa lengo lake asije akajisaidia

sehemu nyingine. Akifanya hivyo hujitahidi kukimbia ili afike sehemu

anakojisaidia. Mnyama huyo kwa jamii ya Ginantuzu humwona kama

akili zake sio nyingi kwani angeweza kujisaidia sehemu nyingine tu. Jina

hili katika koo za Ginantuzu hupewa mtoto wa kiume ambaye anaonekana

ana akili na matendo yanayofanana na mnyama huyo. Lengo pia la

kupewa jina hili ni kumfanya mtoto huyu asifanane na mnyama huyo.

3. Bukela (-a kukosa kitu) Hili ni jina analopewa mtoto wa kike na wazazi wake

kama kiashirio cha mtoto kutokuwa na akili nyingi. Jina hilo hupewa

mtoto huyo baada ya kumwona makuzi ya akili ya mtoto huyo hayapo

sawa na umri wake.

4. Holohondo (panzi jike) Maana halisi ya jina hili ni panzi jike isiyo na mayai.

Kwa kuwa panzi katika koo za Ginantuzi kilikuwa ni kitoweo na panzi

aliyekuwa na thamani sana kwao alikuwa ni panzi jike mwenye mayai

maarufu kama bundikili au buki, panzi jike aliyekosa mayai hakuwa na

mayai. Hivyo basi jina hili aliweza kupewa mtoto wa kiume ambaye

aliashiria kutokuwa na thamani katika familia au jamii yao. Kwa hiyo

muktadha wa jina hili ni mtu yeyote ambaye hakuwa na msaada katika

jamii au familia.

5. Ngokolo (mzembe) Mzembe katika koo za Ginantuzu alionekana kuchukiwa

na watu wote katika ukoo na hata jamii nzina. Jina hili alipewa mtoto wa

kiume ambaye alionekana kuwa mzembe kwa kila hali. Lengo la kupewa

jina hili ni kumtaka ajirekebishe na tabia ya uzembe huo kwani mtu

mzembe katika jamii hiyo alionekana kutokuwa na chochote katika

familia yake. Hali hiyo ilimfanya awe ombaomba wakati wote hali

iliyochukiwa na kila mmoja wakati huo. Mtu mwenye tabia kama hiyo pia

aliweza kupewa jina la Mnyumba yaani mtu anayependa kukaa nyumbani

tu bila kufanya kazi au Ng’olo ikiwa na maaana ya mzembe wa kufanya

kazi yoyote.

6. Makolo (Kondoo) Jina hili alipewa mtoto wa kiume ambaye aliashiria kuwa

mpole kupita kiasi. Mtu ambaye alionekana kuwa hana mchango wa

mawazo katika familia yaani yeye kila kitu anachoambiwa anakubali tu

alifananishwa na kondoo na wakati mwingine alipewa jina la Ng’holo

ikiwa na maana ya kondoo ikidokeza muktadha wa mtu mpole kupita

kiasi.

Jedwali Na. 4.28: Majina Yanayodokeza Uduni

Na. Jina Jinsi Maana yake

1 Budulungu Me Ng’ombe

2 Buga Me Ndege

3 Bukela Me Asiye na akili

4 Butule Me Panzi

5 Ding’ho Me Harufu ya samadi

6 Galedi Me Takataka

7 Golomanda Me Panzi

8 Holohondo. Me Panzi

9 Mnyumba Me Mtu akaaye ndani daima

10 Ndalahwa Me Mdharauliwa

11 Ng’holo Me Kondoo

12 Ng’oba Me Mwoga

13 Ng’olo Me Mzembe

14 Ngokolo Me Mzembe

15 Nhungo Me Mnyama pori jamii ya mbwa

16 Ntengo Me Mtu anayekaa sehemu moja kuhama mpaka aondolewe

17 Sagala Me Hovyo

18 Shagembe Me Buu la nzi linalopatikana kwenye vumbi linyonyalo damu

19 Shunula, Me Mtu akaaye mdomo wazi muda mwingi

Chanzo: Data ya Uwandani – 2017

Data iliyowasilishwa katika Jedwali namba 4.28. hapa juu inadhirisha uwepo wa

majina yaliyotokana na muktadha wa kudokeza udunishaji. Aidha katika jedwali

namba 4.28. hapo juu linaonesha kuwa, majina mengi yaliyokusanywa na mtafiti

akiongozwa na nadharia ya uumbaji kutoka uwandani yameonesha kutumika kwa

wanaume tu. Sababu nyingine ya kutopatiwa majina yanayodokeza uduni ni kulingana

na asili ya mwanamke anavyothaminiwa katika jamii. Hivyo basi, kupatikana kwa

majina ya nayotokana na muktadha wa kudokeza udunishaji kunatimiza moja ya lengo

za Ginantuzu. Aidha, kupatikana kwa data hizi kunadhihirisha kufaa kwa nadharia ya

uumbaji ambayo imetumiwa na mtafiti kama mwongozo wakati wa kukusanya na

kuchambua data za utafiti wake.