• Tidak ada hasil yang ditemukan

Majina ya Watu kwa Kigezo cha Vitendea Kazi Wanavyotumia

4.4 Vigezo Vinavyotumika Kuteua Majina ya Asili katika Koo za Ginantuzu . 104

4.4.1.3 Majina ya Watu kwa Kigezo cha Vitendea Kazi Wanavyotumia

Kama tulivyobainisha hapo mwanzo kuwa baadhi ya majina ya asili katika koo za

Ginantuzu yanatokana na majina ya vitendea kazi wanavyotumia jamii husika. Mtafiti

amebaini kuwa, vitendea kazi ni mojawapo ya vigezo vya utoaji wa majina. Kwa

mujibu wa watafitiwa 28 kati ya 80 waliofikiwa na mtafiti kwa njia ya hojaji na

mahojiano kama ilivyoonesha katika Jedwali Na. 4.4 hapo mwanzo walisema kuwa,

utolewaji wa majina hayo hufungamana na muktadha maalum ambao unaweza kuwa

wa utumiaji au utengenezaji wa vitendea kazi hivyo.

Baadhi ya majina ya asili yaliyoshamili kutokana na vitendea kazi ni pamoja na

Magembe, Isonga, Kasheto, Koloboi, Mapanga, Mbasa, Ilanga, Chenge, Nhunda,

Nungu, Machimu, Izengo, Kisabo, Cheyo, Buta, Mawe, Lukago, Kasuka, Sululu na

Lubiga. Miongoni mwa majina haya, majina yaliyoweza kupatikana karibu kila kata

na kila kijiji ni pamoja na Magembe, Isonga, Ilanga, Kasuka, Mbasa/shoka, Lukago,

Kisabo na Mawe.

Hata hivyo kwa mujibu wa watafitiwa walieleza kuwa utoaji wa majina kwa watoto

kwa kuangalia kigezo cha vitendea kazi umepungua kwa kiasi kikubwa kwani watoto

wanaozaliwa kipindi hiki wanapewa majina yasiyo ya asili na kuacha majina ya asili.

Mtafitiwa mmoja alidai kuwa majina hayo yamepungua kutokana na mabadiliko ya

sayansi na teknolojia kwani baadhi ya vitendea kazi vilivyokuwa vinatumika kutolea

majina kwa sasa zimebadilika. Kubadilika huku kumeathiri kwa kiwango kikubwa

utoaji wa majina kwa kigezo cha vitendea kazi. Hapa chini ni ufafanuzi wa baadhi ya

majina yaliyotokana na kigezo cha vitendea kazi.

1. Magembe (majembe) Jina hili lilitolewa kutokana na upatikanaji wa kitendea

kazi hicho au kutokana na wazazi wa mtoto huyo kuwa

watumiaji wazuri wa kitendea kazi hicho kwani katika jamii ya

2. Isonga (mshale) Hili ni jina ambalo alipewa mtoto wa kiume na wazazi wake

ambaye alizaliwa kipindi cha kutengeneza mishale au wakati

mwingine mshale husika ulikuwa na athari yoyote katika

kuzaliwa kwa mtoto husika. Wakati mwingine mtoto aliweza

kupewa jina hilo kuashiria ushujaa atakaokuwa nao hapo mbele

kwa sababu mshale ulikuwa silaha za kivita.

3. Ilanga (fimbo) Jina hili alipewa mtoto wa kiume aliyezaliwa kipindi cha

kutayarisha fimbo kama silaha. Wakati mwingine fimbo hiyo

iliathiri kwa njia moja au nyingine katika kuzaliwa kwa

mwanzilishi wa jina hilo. Mzee Manyatula mmoja wa watafitiwa

alisema kuwa, baba yake aliitwa jina la Ilanga baada ya mama

yake kushindwa kujifungua chini ya usimamizi wa wakunga wa

kike mpaka wanaume wakiwa na fimbo kumchalaza mpaka

akajifungua salama. Baada ya kujifungua wanawake wenzake

wakawa wanamtania kuwa ‘kujifungua kwako mpaka fimbo’ na mtoto huyo aliyezaliwa aliitwa ‘Ilanga’ ikimaanisha fimbo.

4. Kasuka (jembe) Jina hili alipewa mtoto wa kiume na wazazi wake kipindi cha

kutayarisha majembe tayari kwa kilimo. Wakati mwingine jina

hili aliweza kupatiwa mtoto kama ishara ya ukulima hodari hapo

mbeleni.

5. Mbasa (shoka) Hili ni jina alilopewa mtoto wa kiume ambaye alizaliwa wakati

mama yake akifanya kazi ya kusena au kupasua kuni au kukata

miti porini kwa kutumia kitendea kazi hicho. Kama yalivyo

kutabiri uchapakazi wa mtoto huyo hapo mbeleni kama kilivyo

kifaa chenyewa.

6. Lukago (zindiko) Jina hili alipewa mtoto wa kiume ambaye kuzaliwa kwake

kulikuwa na matatizo yaliyosababishwa na mama kukanyaga

mitego. Hivyo ili kuzaliwa salama ilibidi kufuata miamba wa miti

shamba (wanganga) kwa ajili ya kutegua mitego hiyo na baada ya

kuzaliwa mtoto huyo alipewa jina hilo la zindiko yaani Lukago ili

asiathirike tena na mitego mingine.

7. Kisabo (kibuyu) Hili ni jina alilopewa mtoto wa kiume ambaye alizaliwa

kipindi mama yake akiwa ama anatengeneza kibuyu au kipindi

cha uvunaji wa vibuyu au wakati wa kiangazi kikali ambapo

akina mama wakati wote walikuwa wanatembea na vibuyu kwa

ajili ya kutafuta maji. Wakati mwingine jina hilo lilitokana na

tabia ya mama kuwa anapendelea kubeba kibuyu wakati wa

kufuata maji kipindi cha ujauzito wa mtoto husika.

8. Mawe (mawe) Hili ni jina alilopewa mtoto wa kiume ambaye ama mama yake

alishikwa na uchungu akiwa mlimani au alizaliwa wakati mama

yake akiwa anasaga unga katika mawe kwani kipindi cha zamani

mashine za kusaga unga zilikuwa ni mawe makubwa

yaliyotengenezwa kwa ustadi mkubwa na kutumiwa kama

mashine zilizoendeshwa na akina mama peke yao. Wakati

mwingine mtoto aliweza kupewa jina hilo kutokana na mama

yake kutokuwa na tatizo lolote kipindi chote cha ujauzito wa

9. Chenge (kijinga cha moto) Jina hili alipewa mtoto wa kiume na wazazi wake

ambaye alizaliwa ama kwa wakunga waliomhudumia mzazi

kutumia kifaa hicho (chenge) kama nyenzo ya kupata mwanga

kwa ajili ya kuona kutokana na ukosefu wa taa kipindi hicho au

wakati anazaliwa mtoto huyo kulikuwa na vimulimuli vingi nje

vilivyojulikana kwa jina hilo la chenge vilivyotumiwa na

wachawi au miujiza fulani kuleta athari fulani.

10. Izengo (miti ya kujengea) Hili ni jina alilopewa mtoto wa kiume ambaye

alizaliwa katika kipindi cha kuandaa miti ya kujengea nyumba

ama amezaliwa sehemu ambayo miti hii ya kujengea nyumba

imekusanywa na kuhifadhiwa. Kwa mujibu wa watafitiwa

walisema kuwa hapo zamani nyumba karibu zote zilijengwa kwa

kutumia miti. Sayansi ya kutumia matofari ya udongo na saruji

haikuwepo kabisa.

Kutokana na orodha ya majina yaliyowasilishwa hapo juu inadhihirisha kwamba

baadhi ya majina ya asili katika koo za Ginantuzu yanayotumika maana zake

zinahusiana na majina ya vitendea kazi ambazo zilipatikana kwa wingi katika

mazingira wanamoishi waanzilishi wa majina hayo. Matokeo ya utafiti huu pia

yanadhihirisha kuwa vitendea kazi ni kigezo muhimu kilichozingatiwa katika

kumpatia jina mtoto aliyezaliwa katika koo za Ginantuzu. Katika sehemu hii,

kupatikana kwa majina haya kwa kutumia kigezo cha vitendea kazi vilivyopatikana

katika mazingira waishio, kulitimiza moja ya lengo mahususi la utafiti huu lililolenga

Ginantunzu. Aidha, kupatikana kwa data hizi kunadhihirisha kufaa kwa nadharia ya

uumbaji ambayo imetumiwa na mtafiti kama mwongozo wakati wa kukusanya na

kuchambua data za utafiti huu.