• Tidak ada hasil yang ditemukan

Kigezo cha Ujio wa Vitu Vipya

4.4 Vigezo Vinavyotumika Kuteua Majina ya Asili katika Koo za Ginantuzu . 104

4.4.8 Kigezo cha Ujio wa Vitu Vipya

Jedwali namba. 4.24 hapo juu linaonesha kuwa watafitiwa 5 ambao ni sawa na

asilimia 6.25 wamesema kuwa baadhi ya majina ya asili katika koo za Ginantuzu

hutolewa kutokana na ujio wa vitu vipya. Utafiti unaonesha kuwa ujio wa vitu vipya

ni mojawapo ya vigezo vya utoaji wa majina katika koo za Ginantuzu. Kwa mujibu

wa watafitiwa waliofikiwa na mtafiti kwa njia ya mahojiano walisema kuwa, ujio wa

vitu vipya umekuwa ukitumika sana kutolea majina katika koo za Ginantuzu. Vitu

hivyo vipya vinaweza kuwa viumbe hai au viumbe visivyo hai.

Majina ya watu yanayotolewa kwa kigezo hiki yanatolewa kwa watoto wadogo na

mengine yanatolewa kwa watu wazima kulingana na athari ya kitu hicho katika jamii

husika. Watafitiwa hao walidai kuwa majina haya hutolewa kwa watu kutokana na

kuingia kwa vitu vipya au utawala mpya ambao haukuwepo katika jamii husika.

Watafitiwa pia walisema kuwa lengo la kupatiwa watoto majina hayo ni kuweka

kumbukumbu katika jamii juu ya ujio wa vitu hivyo au utawala huo.

Baadhi ya majina ya asili yaliyoshamiri kutokana na ujio wa vitu vipya ni pamoja na

Tegisi, Mashini, Keya, Dafu, Sikania, Pajero, Nyerere, Ng’winyi, Magufuli, Maseyi, Sadam na Osama. Miongoni mwa majina haya, majina yaliyoweza kupatikana karibu

kila kata na kila kijiji ni pamoja na Mashini, Tegisi, Nyerere, Sadam, Giligita na

Osama. Hata hivyo kwa mujibu wa watafitiwa walieleza kuwa utoaji wa majina kwa

watoto kwa kutumia kigezo cha ujio wa vitu vipya umepungua kwa kiasi kikubwa

kwani watoto wanaozaliwa kipindi hiki wanapewa majina yasiyo ya asili na kuacha

1. Tegisi (basi) Hili ni jina alilopewa mtoto wa kiume baada ya ujio wa basi

yaani gari la abiria. Jina hilo kwa mujibu wa watafitiwa walisema kuwa

mtoto aliweza kupewa jina hilo aidha kwa sababu alizaliwa kipindi cha

ujio wa mabasi hayo au alizaliwa kipindi mama yake akiwa katika basi

akielekea hospitalini kwa ajili ya kujifungulia na akajifungulia humo

humo kwenye basi la abiria kabla ya kufika hospitalini.

2. Nyerere (Rais kwa kwanza wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania) Jina hili

alipewa mtoto wa kiume ambaye alizaliwa kipindi cha utawala wa

kiongozi huyo. Kwa mujibu wa watafitiwa walisema kuwa kutokana na

utawala wa kiongozi huyo kuwa mzuri watoto wengi waliozaliwa

kipindi anaanza kutawala walipewa jina hilo kama ukumbusho kwa

jamii husika. Jina hilo hadi sasa bado linatolewa kwa watoto kutokana

na kurithi kutoka kwa waanzilishi wake.

3. Ng’winyi (Mwinyi Rais wa Jamhuri wa Muungano wa Tanzania awamu ya

pili) Jina hili pia alipewa mtoto wa kiume aliyezaliwa kipindi cha

utawala wa Ali Hassan Mwinyi kama ukumbusho kwa jamii husika.

4. Mashini (mashine) Hili ni jina alilopewa mtoto wa kiume mwanzoni mwa ujio wa mashine za kusaga na kukoboa. Kwa mujibu wa watafitiwa

walisema kuwa hapo mwanzo hapakuwepo na mashine za kusaga unga

na kukoboa nafaka. Kazi hizo zote zilifanywa na wanajamii husika kwa

kutumia nyenzo mbalimbali kama mawe na vinu. Baada ya ujio wa

mashine hizo ilikuwa ni jambo geni sana na watu kipindi hicho

waliweza kukusanyika kwenye mashine hiyo ili kuangalia utendaji kazi

walipatiwa jina la Mashini wakiashiria kuwa watakapokua watoto hao

watakuwa wanafanya kazi kama ilivyo mashine. Kwa hiyo mtoto

aliyepewa jina la Mashini jamii ilitarajia mtoto huyo awe mchapa kazi

sana kama ilivyo mashine.

5. Maseyi (aina ya trekta) Jina hili alipewa mtoto wa kiume ambaye alizaliwa

kipindi cha ujio wa trakta aina ya Massey Furgason. Chombo hiki cha

kilimo hapo mwanzo kiliwashangaza jamii ya Ginantuzu kwa utendaji

kazi wake kwani chombo hiki kiliweza kulima hata kwenye ardhi

iliyoshindikana. Kutokana na chombo hiki, watoto waliozaliwa kipindi

hiki walipewa jina hilo kama ukumbusho. Jina hili halikutolewa kwa

watoto tu bali hata watu wazima walijibatiza kwa jina hili na wengine

wakitumia jina la Giligita ikiwa na maana ile ile ya Trekta.

6. Osama (Kiongozi wa mtandao wa Alkaida) Hili ni jina alilopewa mtoto wa

kiume aliyezaliwa kipindi cha utawala wa mtu huyo. Wakati mwingine

watu wazima walijipatia jina hilo ili kuonesha ubabe alio nao mtu

huyo. Mtu ambaye alionesha hali ya ubabe kipindi kile alistahiri

kupatiwa jina hilo kulingana na matendo aliyokuwa anayafanya.

7. Magufuli (Rais wa awamu ya tano wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania).

Hili ni jina ambalo watoto wa kiume waliozaliwa katika kipindi hiki

cha utawala wa Rais Magufuli wamepewa. Kulingana na majibu ya

watafitiwa walisema kuwa wameamua kutoa jina hilo wakiwa na imani

kuwa hata watoto wao baada ya kukua watakuwa na msimamo na

yalipatikana kwa watoto karibu kila kata na kijiji kilichofikiwa na

mtafiti hasa kwa watoto waliozaliwa kipindi hiki.

Matokeo ya utafiti huu yanadhihirisha kuwa ujio wa vitu vipya wakati mtoto

anazaliwa ni kigezo kingine kilichozingatiwa katika kumpatia jina mtoto anayezaliwa

katika koo za Ginantuzu. Katika sehemu hii, kupatikana kwa majina haya kwa

kutumia kigezo cha ujio wa vitu vipya katika jamii kunatimiza moja ya lengo

mahususi la utafiti huu lililolenga kuonesha vigezo vinavyotumika katika kuteua

majina ya asili katika koo za Ginantunzu. Aidha, kupatikana kwa data hizi

kunadhihirisha kufaa kwa nadharia ya uumbaji ambayo imetumiwa na mtafiti kama

mwongozo wakati wa kukusanya na kuchambua data za utafiti huu.