Utoaji wa majina katika jamii za Afrika ikiwemo Tanzania ni muhimu sana na hubeba
maana si tu katika majina ya watu bali pia hata katika majina ya mahali na vitu.
Watafiti waliotafiti kuhusu majina ya mahali na vitu ni pamoja na Cameroon (1961),
Boas (1964), Hymes (1964), Schotsman (2003), Rugemalira (2005), Buberwa (2010),
na Elihaki (2012).
Cameroon (1961) anaelezea kuhusu utoaji wa majina ya mahali katika jamii ya
Mtaalam huyu katika utafiti wake alibaini aina kuu mbili za majina ya mahali ambayo
ni majina yanayohusiana na makazi na aina ya pili ni majina yanayohusiana na sura ya
nchi kama vile mito na milima. Mtaalamu huyu anaeleza kwamba, watu
wanapoanzisha makazi mahali fulani ambapo awali palikuwa hapaishi watu, hutumia
kigezo cha sura ya nchi ya eneo hilo kutoa jina la mahali hapo. Mtaalam anatoa mfano
wa jina kama vile “Greenhill” likimaanisha eneo lenye kilima chenye ukijani mwingi.
Anaeleza zaidi kwamba kadri makazi yanapoongezeka baadaye majina ya maeneo
mengine huweza kutolewa kutokana na majina ya watu. Utafiti wa mtaalam huyu
umekuwa kichecheo katika utafiti wetu kwa sababu utafiti wetu unahusiana na majina
japo majina tunayoyashughulikia katika utafiti wetu ni majina ya asili katika koo za
Ginantuzu. Kazi ya mtafiti huyu ni muhimu katika utafiti wetu kwani imetupa
muelekeo katika kuchambua majina ya asili katika koo za Ginantuzu.
Boas (1964) anaeleza majina ya mahali katika jamii ya Kwakiutul India kwa kusema
kwamba majina ya mahali huweza kutolewa kutokana na sura ya nchi ya eneo husika
kama vile milima, mabonde, korongo n.k. Pia aliongeza kuwa majina ya mahali
yanaweza kutokana na tabia nchi kama vile baridi sana au mvua nyingi. Majina pia
yanaweza kutokana na nguvu za asili (super natural power). Rangi ni kigezo kingine
kinachotumika kutolea majina ya mahali. Kwa mfano mto “Red river” umepewa jina
hili kutokana na eneo lake kubwa kuwa na rangi (utando) nyekundu.
Ukubwa au udogo wa kitu/eneo ni kigezo kingine kinachoelezwa na mtaalamu huyu
katika utoaji wa majina ya mahali. Akielezea kuhusu lugha na majina ya mahali
na mfumo wa lugha. Ingawa utafiti huu ulijikita katika kuangalia majina ya mahali
katika jamii ya Kwakiutul huko India na kubainisha baadhi ya vigezo vilivyotumika
kupatikana kwa majina hayo kama rangi, ukubwa au udogo wa kitu au eneo. Utafiti
huu umekuwa ni msaada sana katika utafiti wetu kwa sababu, mojawapo ya malengo
mahsusi katika utafiti wetu ni kuonesha vigezo vilivyotumika kuteua majina ya asili
katika koo za Ginantuzu. Hivyo utafiti huu ulitupa dira ya kuchunguza vigezo
vilivyotumika kuteua majina ya asili katika koo za Ginantuzu.
Hymes (1964) naye alizungumzia juu ya majina ya mahali na kueleza kwamba majina
ya mahali yanaakisi fikra za watu, tabia zao na kwa vipindi tofautitofauti. Aliongezea
kwa kusema kuwa majina pia yanaakisi tamaduni na maisha ya watu. Anaeleza
kwamba lugha ni miongoni mwa vipengele muhimu vya utamaduni. Kwa upande wa
mwingiliano wa tamaduni mtaalam huyu anaeleza zaidi kwamba, baadhi ya vipengele
vya utamaduni vinaweza kuchukuliwa kutoka jamii moja kwenda nyingine. Utafiti wa
Hymes (keshatajwa) umekuwa mwanga mkubwa kwetu kwani mojawapo ya matokeo
ya utafiti wetu yalionesha kuwa majina ya asili katika koo za Ginantuzu yanaakisi pia
fikra za mtu, tabia ya mtu na hata utamaduni wa mtu. Hivyo kwa kusoma utafiti huu
umetusaidia sana katika uchambuzi wa data za utafiti wetu.
Schotsman (2003) kwa upande wake alifanya utafiti kuhusu majina ya maeneo katika
mkoa wa Dar es Salaam. Katika uchunguzi wake alijikita katika kuangalia majina ya
vituo vya daladala katika mkoa wa Dar es Salaam. Lengo la uchunguzi wake lilikuwa
kubaini maana na vigezo vilivyotumika kutoa majina ya vituo hivyo. Matokeo ya
tofautitofauti kama vile kuzingatia majengo yaliyopatikana katika maeneo husika
kama vile shule, misikiti, makanisa, majina ya watu maarufu kama vile kituo cha kwa
Mwalimu, majina ya mimea/miti mikubwa kama vile kituo cha Ubungo, jina
lililotokana na mti wa mbungo ambao ulikuwapo katika eneo hilo.
Rugemalira (2005) naye alichunguza majina ya sehemu katika jamii ya Runyambo.
Katika utafiti wake alichunguza mbinu za kimofolojia zinazotumika katika kuunda
majina ya maeneo. Matokeo ya utafiti huo yalibaini kwamba majina katika jamii hiyo
yanaundwa kwa kutumia utaratibu maalum wa kimofolojia. Hata hivyo, utafiti wa
Rugemalira ulijikita kuchunguza majina ya mahali tu tofauti na utafiti wetu
uliochunguza majina ya asili katika koo za Ginantuzu
Buberwa (2010) alitafiti majina ya mahali katika lahaja ya Ruhamba ambayo ni
mojawapo ya lugha ya Kihaya. Lengo la utafiti wake lilikuwa ni kubaini maana na
sababu za kiisimujamii katika utoaji wa majina hayo kwa jamii ya Wahaya. Utafiti
wake ulifanyika katika wilaya ya Bukoba. Matokeo ya utafiti huo yalibaini kuwa
majina ya maeneo katika jamii hiyo yalitokana na vigezo mbalimbali kama vile
maliasili zinazopatikana katika maeneo hayo kama vile milima na mchanga. Jina
kama Mishenye maana yake ni mchanga. Sababu ya kutumia jina hilo ni kutokana na
sehemu husika kuwa na mchanga mwingi. Mfano mwingine ni Mugajwale lenye
maana ya uvivu. Jina hilo lilitolewa kutokana na wakazi wa sehemu husika kuwa na
tabia ya uvivu.
Katika utafiti huo pia alibaini kuwa kuna kategoria saba za majina ya mahali kwa
sehemu za mwiili, majina ya watu, kabila, utaifa wa mtu na kutohoa kutoka lugha
nyingine. Vigezo hivi ndivyo huathiri uitaji wa majina ya sehemu katika jamii ya
Wahamba. Kutokana na tafiti zinazohusu majina ya watu na mahali yenye asili ya
Kiafrika ni wazi kuwa Afrika ina hazina kubwa ya utamaduni uliokitwa katika majina.
Pamoja na kusheheni utajiri huo wa kiutamaduni, bado lugha nyingi za Afrika
hazijafanyiwa utafiti wa kutosha ili kubaini utajiri huo kwa ajili ya maendeleo ya
utamaduni wa Afrika. Utafiti huu utapunguza pengo hili.
Elihaki (2012) naye alichunguza majina ya mahali katika jamii lugha ya Chasu
(Wapare). Mojawapo ya malengo ya utafiti wake yalikuwa kuchunguza maana ya
majina ya mahali katika jamii lugha ya Chasu. Matokeo ya utafiti huo yalibaini kuwa
majina ya mahali katika jamii lugha ya Chasu yana maana. Maana hizo zinatokana na
majina ya watu, koo za watu, wanyama, miti/mimea na maana zingine zinatokana na
matukio mbalimbali.
Matokeo pia yalionesha kuwa majina katika jamiilugha ya Chasu hayakutolewa hivi
hivi bali vigezo vya kiisimujamii kama vile matukio muhimu, tabia na sura ya nchi
zilizingatiwa. Vile vile majina mengine ya mahali katika jamii hii yalitolewa kutokana
na jamii nyingine zilizokuwa na uhusiano na jamii ya Waasu (Wapare).
Hata hivyo, utafiti huu haukuhusika na kuchunguza majina ya mahali kama
walivyochunguza wataalam hawa bali ulichunguza majina ya asili katika koo za
Ginantuzu. Wataalam hawa walitusaidia sana katika kutupa mwanga na njia kuhusu