• Tidak ada hasil yang ditemukan

Tafiti Zinazohusu Majina ya Mahali na Vitu

Utoaji wa majina katika jamii za Afrika ikiwemo Tanzania ni muhimu sana na hubeba

maana si tu katika majina ya watu bali pia hata katika majina ya mahali na vitu.

Watafiti waliotafiti kuhusu majina ya mahali na vitu ni pamoja na Cameroon (1961),

Boas (1964), Hymes (1964), Schotsman (2003), Rugemalira (2005), Buberwa (2010),

na Elihaki (2012).

Cameroon (1961) anaelezea kuhusu utoaji wa majina ya mahali katika jamii ya

Mtaalam huyu katika utafiti wake alibaini aina kuu mbili za majina ya mahali ambayo

ni majina yanayohusiana na makazi na aina ya pili ni majina yanayohusiana na sura ya

nchi kama vile mito na milima. Mtaalamu huyu anaeleza kwamba, watu

wanapoanzisha makazi mahali fulani ambapo awali palikuwa hapaishi watu, hutumia

kigezo cha sura ya nchi ya eneo hilo kutoa jina la mahali hapo. Mtaalam anatoa mfano

wa jina kama vile “Greenhill” likimaanisha eneo lenye kilima chenye ukijani mwingi.

Anaeleza zaidi kwamba kadri makazi yanapoongezeka baadaye majina ya maeneo

mengine huweza kutolewa kutokana na majina ya watu. Utafiti wa mtaalam huyu

umekuwa kichecheo katika utafiti wetu kwa sababu utafiti wetu unahusiana na majina

japo majina tunayoyashughulikia katika utafiti wetu ni majina ya asili katika koo za

Ginantuzu. Kazi ya mtafiti huyu ni muhimu katika utafiti wetu kwani imetupa

muelekeo katika kuchambua majina ya asili katika koo za Ginantuzu.

Boas (1964) anaeleza majina ya mahali katika jamii ya Kwakiutul India kwa kusema

kwamba majina ya mahali huweza kutolewa kutokana na sura ya nchi ya eneo husika

kama vile milima, mabonde, korongo n.k. Pia aliongeza kuwa majina ya mahali

yanaweza kutokana na tabia nchi kama vile baridi sana au mvua nyingi. Majina pia

yanaweza kutokana na nguvu za asili (super natural power). Rangi ni kigezo kingine

kinachotumika kutolea majina ya mahali. Kwa mfano mto “Red river” umepewa jina

hili kutokana na eneo lake kubwa kuwa na rangi (utando) nyekundu.

Ukubwa au udogo wa kitu/eneo ni kigezo kingine kinachoelezwa na mtaalamu huyu

katika utoaji wa majina ya mahali. Akielezea kuhusu lugha na majina ya mahali

na mfumo wa lugha. Ingawa utafiti huu ulijikita katika kuangalia majina ya mahali

katika jamii ya Kwakiutul huko India na kubainisha baadhi ya vigezo vilivyotumika

kupatikana kwa majina hayo kama rangi, ukubwa au udogo wa kitu au eneo. Utafiti

huu umekuwa ni msaada sana katika utafiti wetu kwa sababu, mojawapo ya malengo

mahsusi katika utafiti wetu ni kuonesha vigezo vilivyotumika kuteua majina ya asili

katika koo za Ginantuzu. Hivyo utafiti huu ulitupa dira ya kuchunguza vigezo

vilivyotumika kuteua majina ya asili katika koo za Ginantuzu.

Hymes (1964) naye alizungumzia juu ya majina ya mahali na kueleza kwamba majina

ya mahali yanaakisi fikra za watu, tabia zao na kwa vipindi tofautitofauti. Aliongezea

kwa kusema kuwa majina pia yanaakisi tamaduni na maisha ya watu. Anaeleza

kwamba lugha ni miongoni mwa vipengele muhimu vya utamaduni. Kwa upande wa

mwingiliano wa tamaduni mtaalam huyu anaeleza zaidi kwamba, baadhi ya vipengele

vya utamaduni vinaweza kuchukuliwa kutoka jamii moja kwenda nyingine. Utafiti wa

Hymes (keshatajwa) umekuwa mwanga mkubwa kwetu kwani mojawapo ya matokeo

ya utafiti wetu yalionesha kuwa majina ya asili katika koo za Ginantuzu yanaakisi pia

fikra za mtu, tabia ya mtu na hata utamaduni wa mtu. Hivyo kwa kusoma utafiti huu

umetusaidia sana katika uchambuzi wa data za utafiti wetu.

Schotsman (2003) kwa upande wake alifanya utafiti kuhusu majina ya maeneo katika

mkoa wa Dar es Salaam. Katika uchunguzi wake alijikita katika kuangalia majina ya

vituo vya daladala katika mkoa wa Dar es Salaam. Lengo la uchunguzi wake lilikuwa

kubaini maana na vigezo vilivyotumika kutoa majina ya vituo hivyo. Matokeo ya

tofautitofauti kama vile kuzingatia majengo yaliyopatikana katika maeneo husika

kama vile shule, misikiti, makanisa, majina ya watu maarufu kama vile kituo cha kwa

Mwalimu, majina ya mimea/miti mikubwa kama vile kituo cha Ubungo, jina

lililotokana na mti wa mbungo ambao ulikuwapo katika eneo hilo.

Rugemalira (2005) naye alichunguza majina ya sehemu katika jamii ya Runyambo.

Katika utafiti wake alichunguza mbinu za kimofolojia zinazotumika katika kuunda

majina ya maeneo. Matokeo ya utafiti huo yalibaini kwamba majina katika jamii hiyo

yanaundwa kwa kutumia utaratibu maalum wa kimofolojia. Hata hivyo, utafiti wa

Rugemalira ulijikita kuchunguza majina ya mahali tu tofauti na utafiti wetu

uliochunguza majina ya asili katika koo za Ginantuzu

Buberwa (2010) alitafiti majina ya mahali katika lahaja ya Ruhamba ambayo ni

mojawapo ya lugha ya Kihaya. Lengo la utafiti wake lilikuwa ni kubaini maana na

sababu za kiisimujamii katika utoaji wa majina hayo kwa jamii ya Wahaya. Utafiti

wake ulifanyika katika wilaya ya Bukoba. Matokeo ya utafiti huo yalibaini kuwa

majina ya maeneo katika jamii hiyo yalitokana na vigezo mbalimbali kama vile

maliasili zinazopatikana katika maeneo hayo kama vile milima na mchanga. Jina

kama Mishenye maana yake ni mchanga. Sababu ya kutumia jina hilo ni kutokana na

sehemu husika kuwa na mchanga mwingi. Mfano mwingine ni Mugajwale lenye

maana ya uvivu. Jina hilo lilitolewa kutokana na wakazi wa sehemu husika kuwa na

tabia ya uvivu.

Katika utafiti huo pia alibaini kuwa kuna kategoria saba za majina ya mahali kwa

sehemu za mwiili, majina ya watu, kabila, utaifa wa mtu na kutohoa kutoka lugha

nyingine. Vigezo hivi ndivyo huathiri uitaji wa majina ya sehemu katika jamii ya

Wahamba. Kutokana na tafiti zinazohusu majina ya watu na mahali yenye asili ya

Kiafrika ni wazi kuwa Afrika ina hazina kubwa ya utamaduni uliokitwa katika majina.

Pamoja na kusheheni utajiri huo wa kiutamaduni, bado lugha nyingi za Afrika

hazijafanyiwa utafiti wa kutosha ili kubaini utajiri huo kwa ajili ya maendeleo ya

utamaduni wa Afrika. Utafiti huu utapunguza pengo hili.

Elihaki (2012) naye alichunguza majina ya mahali katika jamii lugha ya Chasu

(Wapare). Mojawapo ya malengo ya utafiti wake yalikuwa kuchunguza maana ya

majina ya mahali katika jamii lugha ya Chasu. Matokeo ya utafiti huo yalibaini kuwa

majina ya mahali katika jamii lugha ya Chasu yana maana. Maana hizo zinatokana na

majina ya watu, koo za watu, wanyama, miti/mimea na maana zingine zinatokana na

matukio mbalimbali.

Matokeo pia yalionesha kuwa majina katika jamiilugha ya Chasu hayakutolewa hivi

hivi bali vigezo vya kiisimujamii kama vile matukio muhimu, tabia na sura ya nchi

zilizingatiwa. Vile vile majina mengine ya mahali katika jamii hii yalitolewa kutokana

na jamii nyingine zilizokuwa na uhusiano na jamii ya Waasu (Wapare).

Hata hivyo, utafiti huu haukuhusika na kuchunguza majina ya mahali kama

walivyochunguza wataalam hawa bali ulichunguza majina ya asili katika koo za

Ginantuzu. Wataalam hawa walitusaidia sana katika kutupa mwanga na njia kuhusu