• Tidak ada hasil yang ditemukan

Muktadha wa Kudokeza Mahusiano katika Familia

4.5 Miktadha ya Majina ya Asili katika Koo za Ginantuzu

4.5.5 Muktadha wa Kudokeza Mahusiano katika Familia

Kama ilivyoelezwa hapo mwanzo kuwa, mahusiano ni hali ya kushirikiana au

kutoshirikiana katika mambo mbalimbali katika jamii ya watu. Mahusiano hayo

yanaweza kuwa mazuri (kushirikiana) au mabaya (kutoshirikiana). Mahusiano katika

familia ni muktadha unaotumika kuelezea majina ya asili katika koo za Ginantuzu.

Katika utafiti huu imebainika kuwa majina yaliyo mengi katika koo za Ginantuzu

yamedokeza muktadha wa mahusiano yaliyopo ndani ya familia na jamii kwa ujumla.

Majina ya aina hii yanaeleza mahusiano halisi yaliyo katika jamii husika. Majina hayo

mengine yanaonesha muktadha wa upendo, amani, furaha na mengine yamedokeza

chuki, ugomvi, mgogoro na migongano katika jamii husika. Kwa mujibu wa

watafitiwa hao waliendelea kusema kuwa mahusiano katika jamii yanaweza kuwa

mazuri na kwa upande mwingine yasiwe mazuri. Mahusiano yote hayo hujibainisha

katika majina wanayowapa watoto wao. Majina yanayopatikana kutokana na

mahusiano mazuri huwa yako wazi na ya kueleweka katika jamii lakini majina

yanayopatikana kutokana na mahusiano mabaya mara nyingi huwa na mafumbo ndani

yake. Baadhi tu ya majina yanayodokeza muktadha wa mahusiano katika familia ni

pamoja Mayombo, Mlekwa, Masanja, Buyegi, Lusangija, Mpejiwa, Oleng’wa,

Mihayo, Buki, Mpelwa, Matulanya, Mababza na Maseko.

Katika majina hayo, watafitiwa walifafanua kwa kueleza kuwa majina kama

yanadokeza muktadha wa mahusiano mazuri katika familia husika. Kwa mfano jina

Maseko ni jina analopewa mtoto wa kiume na wazazi wake wakiashiria kuwa mtoto

huyo amezaliwa kipindi cha amani katika familia hiyo. Hata wazazi wa mtoto huyo

wanaamini kuwa mtoto, huyo naye atakuwa ni mtu mwenye amani tele katika maisha

yake. Jina Oleng’wa lenye maana ya kukataliwa ni jina alilopewa mtoto wa kiume na wazazi wake baada ya muda mfupi kuzaliwa na mmojawapo ya wanandoa hao hasa

baba au familia anakoishi mama wa mtoto huyo kumkataa mtoto huyo. Jina hilo

hudokeza muktadha wa mahusiano mabaya. Majina mengine ambayo yanatawala sana

katika koo za Ginantuzu yenye kuonesha uhusiano mbaya ni Mlekwa lenye maana ya

aliyeachwa, Mpelwa lenye maana ya aliyekimbiwa na Masolwa lenye maana ya

aliyeokotwa. Majina haya ni baadhi tu ya majina ambayo yanadokeza muktadha wa

mahususiano mabaya katika familia mpaka ikafikia mmojawapo wa wazazi kuamua

kumwacha, kumkimbia au kumtupa kabisa mtoto. Matendo hayo yanapotokea katika

jamii watu wenye jukumu la kutoa majina kwa mtoto kumpatia mtoto jina hilo la

Masolwa kama alitupwa, Mlekwa au Mpelwa kama aliachwa au alikimbiwa na mzazi

wake. Hapa tunapenda kukufahamisha kuwa si kila mwenye majina hayo alitokea

katika muktadha huo hasha, majina haya wengine hupewa kutokana na kurithi kama

kumbukumbu kutoka kwa wanzilishi wake ambao asili yake alitokana na muktadha

huo. Hapa chini ni ufafanuzi wa baadhi ya majina hayo majina hayo.

1. Mayombo (vurugu) Jina hili alipewa mtoto wa kiume na wazazi wake ambaye

alizaliwa kipindi cha vurugu ya kijamii au kifamilia au muda mfupi baada

ya kipindi hicho cha vurugu. Watafitiwa pia walisema kuwa jina hili

linaweza kuwa Kayombo kama vurugu iliyotokea katika familia husika

2. Lusangija/Masanja (unganisha) Hili ni jina analopewa mtoto wa kiume na

wazazi wake baada ya kuzaliwa au kabla ya kuzaliwa kulikuwa na

vurugu kati ya mme na mke kiasi kwamba walikuwa wametengana.

Mara nyingi utenano huo ulisababishwa na kutopata mtoto. Katika koo

za Ginantuzu mtoto ni kiungo kikubwa cha kudumisha ndoa. Hali ya

kutopata mtoto kwa wanandoa husababisha vurugu isiyo na kikomo.

Baada ya kupata mtoto, mtoto huyo huwafanya waliotengana wawe

pamoja na jina la mtoto huyo aliyewaunganisha mtoto wazazi hao

hupewa jina la hujulikana kwa kwa jina la Lusangija/Sangija/Masanja

lenye kudokeza muktadha wa kurejea kwa mahusiano mazuri

yaliyopotea.

3. Mpejiwa (aliyefukuzwa) Jina hili alipewa mtoto ambaye mama yake

alifukuzwa na mme au familia mara tu baada ya kuzaliwa mtoto huyo.

Jina hili lilitolewa na wazazi wa mtoto huyo kutokana na vurugu

iliyotokea katika familia hiyo kama kumbukumbu ya baadaye kwa ajili

ya tukio hilo alilofanyiwa. Kwa hiyo basi jina hili linadokeza muktadha

wa kuwepo na mfarakano baina ya wanafamilia husika. Jina hili pia

liliweza kurithiwa kutoa kwa mwanzilishi ambaye ilimtokea hali hiyo.

Hivyo si kila mwenye jina hili kuna muktadha wa mfarakano bali

wengine hupewa jina hilo kwa ajili ya kumbukumbu tu.

4. Buyegi (furaha) Hili ni jina analopewa mtoto wa kike na wazazi wake au

jamii yake hasa baada ya mtoto huyo kuzaliwa na kuikuta familia ya

mtto huyo ikiwa katika kipindi cha furaha. Kama mtoto wa kiume

furaha pia. Hivyo jina hilo linadokeza muktadha wa amani katika familia

ya huyo mtoto kwani jina Buyegi linaweza kudokeza furaha kwa mtoto

ama furaha kwa familia. Wakati mwingine jina hilo hupatiwa mtoto na

wazazi wake wakimtabiria mtoto huyo kuwa na furaha katika maisha

yake.

5. Mihayo (maneno) Jina hili hupewa mtoto wa kiume au wa kike na watoa jina

wakiashiria kuwa aidha kipindi mama yake akiwa na ujauzito wa mtoto

huyo alikumbana na msukosuko wa vita vya maneno toka ama kwa

mme, ndugu, jamaa, jamii au hata familia yake kiasi kwamba mama

huyo alipata wakati mgumu sana kwa kipindi chote cha ujauzito. Hivyo

basi, baada ya kujifungua mtoto huyo watoa jina ikabidi wampatie jina

hilo ili kusadifu yaliyompata kipindi cha ujauzito kama kumbukumbu.

Wakati mwingine jina hilo lilitolewa kwa mtoto ikiwa mama wa mtoto

huyo alikuwa mwongeaji kupita kiasi yaani alikuwa haishiwi na maneno

kipindi cha ujauzito wake mpaka ikawalazimu watoa jina kumpatia jina

hilo kama kumbukumbu. Kwa maana hiyo jina hilo linadokeza pia

muktadha wa kutokuwa na amani katika familia husika.

6. Matulanya (mchonganishi) Hili ni jina ambalo hupewa mtoto wa kiume na

wazazi wake kukiwa na vurugu ya uchonganishi katika familia husika.

Vurugu hiyo itakuwa imesababishwa na mtoto huyo aliyezaliwa kwa njia

moja au nyingine. Wakati mwingine vurugu ya uchonganishi huo huwa

kwa mmojawapo wa wazazi wake. Kutokana na vurugu hiyo mtoto

hupewa jina hilo ili kutunza kumbukumbu ya tukio hilo la vurugu

mzima. Mara nyingi mtu huyo aliyepewa jina hilo huwa na tabia ta

uchonganishi miongoni mwa wanajamii.

7. Maseko (kicheko) Jina hili hupewa mtoto wa kiume aliyezaliwa kipindi cha

amani na furaha kiasi kwamba kuzaliwa kwa mtoto huyo kulileta

kicheko ndani ya familia na jamii kwa ujumla. Jina hili hubadilika na

kuwa Nsekela kama mtoto atazaliwa wa kike katika kipindi hicho likiwa

na maana hiyo hiyo. Hivyo basi jina hili nalo hudokeza muktadha wa

amani na furaha katika familia husika.

8. Mapambano (mapambano) Hili ni jina analopewa mtoto wa kiume ambaye

amezaliwa kipindi cha mapambano fulani. Mapambano hayo yanaweza

yakawa ya kifamilia, kiukoo au kijamii Jina jingine katika koo za

Ginantuzu linalofanana na hilo ni Bulugu. Hivyo basi jina hili la

Mapambano hudokeza mukiadha wa kutokuwa na amani wakati mtoto

huyo anazaliwa aidha katika familia hiyo au katika jamii hiyo.

9. Mabanza (mashitaka) Hili ni jina ambalo anapewa mtoto wa kiume ambaye

alizaliwa kipindi cha mashitaka baina ya wanadoa au wanajamii husika.

Wakati mwingine jina hili hupewa mtoto ambapo mmoja wapo wa

wazazi wake kama baba au mama alikuwa na tabia ya kupenda sana kesi.

Hivyo basi jina hili hudokeza pia muktadha wa kutokuwa na amani

katika jamii ya mtoto huyo.

Kutokana na majina hayo, utafiti umebaini kuwa majina ya watu katika koo za

Ginantuzu hudokeza muktadha wa mahusiano yaliyopo katika familia na jamii kwa