• Tidak ada hasil yang ditemukan

Kwa kawaida, data za utafiti wa kimaelezo hupatikana katika muundo wa maneno na

siyo namba (idadi). Ili kuhakikisha kuwa data za utafiti huu ni thabiti na halali kwa

kiwango cha kuridhisha, mbinu tofautitofauti za kukusanya data zilitumiwa. Katika

utafiti huu mtafiti alitumia mbinu ya hojaji na mbinu ya mahojiano kwa kukusanya

data za msingi kwenye uwanda wa utafiti. Mtafiti alitumia mbinu hizi mchanganyiko

kwa lengo la kupata matokeo yaliyo bora. Kama walivyobainisha na Best na Khan

(1993) kwamba, mbinu moja haijitoshelezi katika kupata data zinazoaminika na

kukubalika katika utafiti. Lengo la mtafiti kutumia mbinu hizi ni kwamba; Kwanza,

ni kupata uthabiti wa matokeo ya utafiti aliokusudia kuufanya. Pili, mbinu hizi

zilimsaidia kukusanya data kwa haraka na kwa wingi. tatu, mbinu hizi zilimsaidia

3.7.1 Hojaji

Hojaji ni miongoni mwa mbinu zinazotumika kukusanyia data. Kwa mujibu wa

Kothari (2004) hojaji ni mbinu ya kukusanyia data ambapo mtafiti huandika maswali

na kisha kuyapeleka kwa watoa taarifa ili wayajibu na baadae kumrudishia mtafiti

yakiwa tayari yemeshajibiwa. Mbinu hii ilitumiwa sana kwa watafitiwa lengwa ambao

wanajua kusoma na kuandika. Aidha, mbinu hii ilitumika ili kuhakiki, kulinganisha,

na kuthibitisha data zilizotokana na mapitio ya nyaraka ili kupata mtazamo kuhusu

makundi ya majina ya asili, vigezo vilivyotumika kuteua majina ya asili na miktadha

ya majina ya asili katika koo za Ginantuzu.

Mbinu hii ilitumika kujibu maswali yote matano ya utafiti wetu, Hojaji ilitumika kwa

Sampuli ya jamii ya Ginantuzu wenye umri wa kuanzia miaka 25 – 85 ambao idadi

yao walikuwa 40, yaani vijana 20 wenye umri wa miaka 25-54 kwa uwiano sawa wa

kijinsia na wazee 20 wenye umri kuanzia miaka 55-85 kwa uwiano sawa wa kijinsia.

Mbinu hii iliwapa fursa watafitiwa hao kutoa maelezo ya kina na yenye hoja za

kitaaluma. Mbinu ilimsaidia mtafiti kupata taarifa mbalimba kuhusu makundi ya

majina ya asili, vigezo vilivyotumika kuteua majina ya asili na miktadha mbalimbali

ya majina ya asili katika koo za Ginantuzu kupitia maswali yote yaliyoandaliwa na

mtafiti. Faida zifuatazo tulizipata kwa kutumia mbinu hii:

(i) Mbinu hii ilimsaidia mtafiti kwa kuwa ina gharama ndogo na ni rahisi kutumika

kupata taarifa nyingi kwa muda mfupi.

(ii) Mbinu hii iliweza kuibua taarifa nyingi na ilimsaidia mtafiti kukusanya data

(iii) Mbinu hii ilimpa mtafitiwa uhuru wa kujieleza na kujaza kile anachokifahamu

kulingana na uwezo, uelewa na tajiriba yao kuhusu maswali aliyoulizwa kwenye

hojaji.

(iv) Mbinu hii ilikuwa na hojaji iliyoandaliwa ikiwa na orodha ya maswali sawa na

yanayofanana kwa watafitiwa wote ili kumsaidia mtafiti kufanya ulinganifu wa

majibu kutoka kwa watafitiwa.

Aidha aina ya data zilizokusanywa katika njia hii ya hojaji ni data za msingi. Hapa

mtafiti aliorodhesha maswali aliyotaka yajibiwe na watafitiwa na kuyapeleka

uwandani. Maswali hayo yote yalilenga kujibu vipengele vya makundi ya majina ya

asili katika koo za Ginantuzu, vigezo vilivyotumika kuteua majina ya asili katika koo

za Ginantuzu na miktadha ya majina ya asili katika koo za Ginantuzu. Majibu ya

maswali hayo yaliweza kutimiza malengo mahususi matatu ya utafiti. Katika njia hii,

jumla ya watafitiwa 40 tu kutoka katika vijiji vyote 10 ndio waliohusishwa, kwa kuwa

ndio waliokuwa wanajua kusoma na kuandika. Aidha watafitiwa wote 40 walirejesha

majibu yao, tena kwa wakati uliopangwa. Pamoja na mafanikio makubwa

yaliyopatikana katika mbinu ya hojaji kulikuwa na kasoro zifuatazo kama baadhi ya

watafitiwa uandishi wao ulikuwa haufahamiki. Pia watafitiwa ambao walikuwa

hawajui kusoma na kuandika walishindwa kutoa taarifa za utafiti. Kutokana na

watafitiwa kutojua kusoma na kuandika, mtafiti alitumia mbinu ya mahojiano ili

kuweza kuziba kasoro hizo ziliyojitokeza.

3.7.2 Mahojiano

Mahojiano (usaili) ni majibizano ya ana kwa ana, simu, dijitali au barua pepe kati ya

watu wawili au zaidi kwa lengo la kukusanya taarifa au maoni kuhusu suala fulani la

kufanywa kwa simu, dijitali au barua pepe, uulizaji wa maswali ya ana kwa ana au

majadiliano ndio uliotumika zaidi katika utafiti huu. Aidha aina ya data

zilizokusanywa katika njia hii ya mahojiano ni data za msingi. Katika mbinu hii,

wahojiwa 20 wenye umri kati ya 25-54 na wahojiwa 20 wenye umri kati ya 55-85

kutoka sampuli ya watu 40 walifikiwa na mtafiti. Mbinu hii ilitumiwa kwa watu 40.

Mtafiti aliichagua njia hii kwa sababu zifuatazo:

(i) Mbinu hii ilitoa fursa kwa watafitiwa ambao hawajui kusoma na kuandika

kuweza kushiriki katika kutoa taarifa za kutosha na za kina kuhusu utafiti.

(ii) Mbinu hii ilimsaidia mtafiti kupata taarifa nyingine ambazo zisingepatikana kwa

mbinu ya hojaji.

(iii) Mbinu hii ilitoa fursa ya kuuliza maswali ya ziada na kujibu maswali

tokezi/ibukizi yaliyojitokeza katika mahojiano kati ya mtafiti na mtafitiwa.

(iv) Njia hii pia ilimsaisia mtafitiwa kuelewa swali ipasavyo kwani ni mbinu pekee

inayotoa fursa kwa mtafiti kutoa maelezo zaidi kwa swali ambalo halikueleweka

kwa mtafitiwa.

(v) Njia hii inatoa mwanya kwa maswali mengine ya kujieleza yaani maswali

ambayo yako nje ya yale yaliyoulizwa (maswali ibukizi).

(vi) Mbinu hii ilimpa fursa mtafitiwa kueleza hisia zake binafsi kuhusu mada

inayotafitiwa.

Mbinu ya mahojiano ilimwezesha mtafiti kukusanya data zilizohusiana na makundi ya

majina, vigezo walivyotumia kuteua majina na mazingira yanayopelekea watu

kupewa majina ya asili katika koo za Ginantuzu. Hivyo basi, mchakato wa mahojiano

upatikanaji wa watafitiwa. Mahojiano yaliendeshwa kwa lugha ya Kiswahili kwa

watafitiwa wanaoweza kutumia lugha ya Kiswahili. Watafitiwa walioshindwa

kutumia lugha ya Kiswahili mahojiano yaliendeshwa kwa lugha ya Ginantuzu kwa

kuwa mtafiti naye ni mzungumzaji wa lugha ya Ginantuzu. Data zilizopatikana katika

mbinu hii zilinukuliwa na kuhifadhiwa kwa lugha ya Kiswahili kwa njia ya

maandishi.