• Tidak ada hasil yang ditemukan

Muktadha wa Kudokeza Tabia na Matendo

4.5 Miktadha ya Majina ya Asili katika Koo za Ginantuzu

4.5.7 Muktadha wa Kudokeza Tabia na Matendo

Majina yanayotokana na muktadha wa tabia na matendo ya mtu kwa kawaida huakisi

mienendo ya wahusika. Mienendo hiyo hujumuisha ubishi, ukaidi, uasherati,

majivuno, usafi, hasira, upole, uchoyo, ukali, ubishi, ulevi na ukorofi. Watafitiwa

walibainisha kuwa muktadha wa tabia na matendo ya mtu hudokezwa katika majina

ya asili katika koo za Ginantuzu. Tabia na matendo hayo yalifanywa na waanzilishi

wa koo husika katika jamii. Matendo hayo katika jamii yalitofautiana kati ya mtu

mmoja na mwingine kama anavyodai Adrey (1970) kwamba, kila mtu katika jamii

ana tabia na matendo yanayoweza kumtofautisha na wengine. Madai haya yaliungwa

matendo yanayoweza kumtofautiasha na wengine. Utafiti umebaini kuwa katika koo

za Ginantuzu, kuna majina ya asili yenye maana yatokanayo na tabia na matendo ya

watu. Baadhi ya majina yanayotokana na tabia na matendo ya mtu ni pamoja na

Mabiti/Mbiti, Ng’homi, Salisali, Magulyati, Shayayi, Mbogo, Pilipili, Mashimba/ Shimba, Kitalumba, Ngokolo, Kuyela, Masemba, Nkwabi, Lombiha, Kuyela,

Ng’walali na Long’we. Katika majina haya yaliyoorodheshwa hapa juu, majina kama Mabiti/ Mbiti, Ng’homi, Salisali, Magulyati, Shayayi, Mbogo, Pilipili, Mashimba/Shimba, Kuyela, Walwa, Mahela, Ngokolo, Nkwabi na Masemba

yalionekana kutumiwa sana katika koo za Ginantuzu kwa sababu kila kata iliyofikiwa

na mtafiti kulikuwepo na uwepo wa majin haya. Majina haya yana maana fulani

katika jamii. Lengo kuu la kupewa majina hayo katika jamii ni kuwafanya wanajamii

waendelee na tabia na matendo yao yanayokubalika katika jamii au wajirekebishe na

tabia na matendo yasiyokubalika katika jamii husika.

Kwa mujibu wa watafitiwa walisema kuwa majina hayo yalitolewa kwa watoto wao

kwa ajili ya kuhimiza au kupinga tabia na matendo mabovu pindi watakapokuwa

wakubwa. Hapa chini ni ufafanuzi wa maadhi ya majina yaliyotokana na muktadha

wa tabia na matendo ya watu.

1. Mabiti (fisi) Hili ni jina analopewa mwanaume ambaye alikuwa na tabia na

matendo kama ya mnyama fisi. Jina hili linadokeza muktadha ya mtu aliye

na tamaa kupita kiasi. Jina hili wakati mwingine hujulikana kama Mbiti.

Vilevile kupatikana kwa wingi kwa mnyama huyu au mnyama huyu kuwa

na athari fulani katika maeneo husika katika jamii ni muktadha mwingine

2. Ng’homi (nge) Jina hili hupewa mwanaume ambaye ana tabia na matendo ya

ukali wa kupindukia kama alivyo mdudu nge. Hivyo jina hili hudokeza

mtu mkali na kaidi kuliko kawaida ya watu wengine. Tena watu wengine

mtu mwenye jina hili humwoona hatari sana katika jamii husika.

3. Salisali (panzi) Salisali ni panzi ambaye hachoki kuruka na panzi huyu pia ni

mjanja kuliko panzi wengine. Hivyo jamii katika koo za Ginantuzu

huamua kumpatia jina hili mwanaume ambaye ni mjanjamjanja katika

jamii. Wakati mwingine mtu mwenye tabia na matendo ya namna hiyo

humwiita mapepe ambaye hashikiki wala kukamatika.

4. Shayayi (sungura) Jina hili hupewa mwanaume ambaye anatabia na matendo ya

ujanjaujanja kama sungura alivyo. Mtu mwenye matendo haya katika

jamii ya Ginantuzu huwa hapendwi na jamii nzima. Hivyo mtu hupewa

jina hilo ili ajirekebishe na tabia ya ujanja ujanja.

5. Mbogo (nyati) Jina hili hupewa mtu wa kiume ambaye ni mpole katika jamii

lakini ni hatari sana ukimkorofisha. Tabia na matendo ya mnyama huyu

hupendwa sana na jamii katika koo za Ginantuzu. Jina hili katika jamii ya

Ginantuzu linatawala sana na kila mmoja anajivunia kuwa nalo katika

jamii.

6. Pilipili (pilipili) Kama lilivyo jina lenyewe pilipili kuwa ni kali. Hivyo jina hili

hupewa mtoto wa kiume ambaye anaonekana kuwa hapendi matani katika

jamii. Hivyo basi, jina hili hudokeza muktadha wa ukali na mtu

anayepewa jina hili husadifu jina lenyewe. Majina mengine

7. Kuyela (kuzurula) Hili ni jina analopewa mwanaume ambaye alionekana kuwa

na tabia na matendo ya uzururaji. Tabia ya uzururaji katika koo za

Ginantuzu ilipigwa vita sana hapo zamani kwani mtu wa namna hiyo

hakuwa na maendeleo yoyote kwake na hata katika jamii yake.

8. Masemba (vituko/utani) Hili ni jina alilopewa mtoto wa kiume na wazazi wake. Mtu ambaye alikuwa na vituko sana au mwazilishi wa jina hilo

alikuwa na vituko vingi vyenye kushangaza na kuchekesha katika maisha

yake, alistahiri jina hilo. Watu wenye vituko katika jamii ya Ginantuzu

kwa kiasi kikubwa walipendwa sana na walitakiwa sana kuwepo katika

shughuli yoyote iliyokuwa inafanywa kwa jumuia. Hivyo mtoto aliweza

kupewa jina hili kama ukumbusho wa mwanzilishi huyo.

9 Nkwabi (mtafutaji mali) Jina hili alipewa mtoto wa kiume akirithi kutoka kwa

wazazi/waanzilishi. Mwanzilishi wa jina hili alipewa kutokana na tabia ya

utafutaji mali kwa njia halali. Katika jamii ya Ginantuzu mtu kama huyu

alipendwa na kila mtu mwenye moyo wa utafutaji mali. Utafutaji mali

ulikuwa ni msingi wa maisha katika koo za Ginantuzu hivyo jina kama

hili lilipendwa na jamii na linapatikana kwa wingi katika koo za

Ginantuzu mpaka sasa.

10 Mayumila (kutoa kitu bila kipimo maalum) Jina hili lilitolewa kwa mtoto wa

kiume akirithi kutoka kwa mwanzilishi aliyekuwa na matendo na tabia

nzuri iliyokubalika kwa jamii kiasi kwamba alikuwa anatoa kitu chochote

kwa watu wengine bila kutumia kipimo maalum. Tabia kama hii ilikuwa

inamilikiwa na wachache sana. Wachache hawa walipewa jina hili kama

hulifupisha na kuliita Mayuma. Hivyo jina hili hudokeza muktadha wa

ukarimu kwa watu wengine.

Kutokana na ufafanuzi wa majina hayo hapa juu, utafiti umebaini kuwa tabia na

matendo ya mtu unadokeza muktadha wa majina katika koo za Ginantuzu na

muktadha huo wa majina huwa na maana tu kwa jamii husika. Mtoto anayepewa jina

la aina hiyo kutambuliwa kuwa yeye ni Mnyantuzu kutokana na jina la Ginantuzu

linalomtambulisha kwa jamii yake.

Ningependa ifahamike kuwa miktadha iliyoelezwa na watafitiwa ni baadhi tu kwani

ipo miktadha mingi kulingana na sehemu ambako mtoto alipewa hilo jina. Wakati

mwingine athari fulani ya jina halisi katika mazingira ya mtoto yaliweza kuchangia

kumaanisha maana ya jina husika. Hivyo basi jamii katika koo za Ginantuzu ziliweza

kutoa jina kulingana na miktadha mbalimbali.