• Tidak ada hasil yang ditemukan

2.5 Kiunzi cha Nadharia

2.5.1 Nadharia ya Uumbaji

Nadharia ya Uumbaji iliasisiwa na mwanaisimu wa Kimarekani Edward Sapir (1958)

na kuendelezwa na mwanafunzi wake Benjamin Lee Whorf (1958) ambaye baadaye

mwanafunzi huyo alidai kuwa ni yake na akaiita Dhanio la Whorf. Mpaka sasa

wataalam wengi wa isimu wanaiita kama nadharia jumuishi ya Sapir - Whorf.

Kimsingi nadharia hii inahusu lugha na utamaduni. Sapir aliamini kuwa upo uhusiano

wa lugha na jamii na kusema kuwa lugha hutawala fikra za wazungumzaji wake na

kuwapa namna ya kuusawiri ulimwengu wao. Sapir (keshatajwa) anaendelea kwa

kusema kwamba lugha ndio msingi wa kuuelewa ulimwengu. Unapojifunza lugha ni

na dunia kama ilivyoratibiwa na wasemaji wake. Binadamu huuona ulimwengu

kupitia taratibu zilizowekwa na lugha yake ya kwanza. Ni vigumu kuchukua jina la

mtu kutoka katika jamii fulani na kumpa mtu wa jamiilugha nyingine kwa sababu jina

la jamii moja hufungamana na imani hiyo ambayo huambatana na utamaduni wa jamii

husika. Kutokana na maelezo hayo watu wenye misingi tofauti ya lugha hawapati

picha sawia ya ulimwengu. Ulimwengu tunamoishi kwa kiasi kikubwa umejengwa

kupitia lugha za jamii fulani. Jamii zinatofautiana katika kujenga fikra na mawazo

kutokana na vitu mbalimba katika lugha husika kama ilivyo kwa majina ya asili ya

jamiilugha moja na nyingine ulimwenguni hususani Barani Afrika. Sapir (1921)

anaeleza kuwa, wanadamu hawaishi katika ulimwengu dhahiri wala wa pekee bali

wanazungukwa na shughuli za kijamii na kuzama katika ulimwengu wa lugha ambao

ndio njia pekee ya kujieleza katika jamii. Lugha huakisi ulimwengu halisi kwa kiasi

kikubwa na ulimwengu wa lugha umefungamana na tabia za lugha ya kundi au jamii

fulani. Watu huona, husikia na huwa na tajiriba ya mazingira yao kwa kuchukulia

kuwa lugha zao hufafanua na kuelezea tajiriba zao na hivyo, huathiri maisha yao.

Maoni ya Sapir yaliungwa mkono na Whorf aliposema kuwa wazungumzaji wa lugha

zilizo na sarufi tofauti huelekezwa na sarufi za lugha zao kwa njia tofauti ya kuyaona

mambo hayo. Whorf alifanya utafiti kwa kuchunguza lugha ya mzungumzaji mmoja

wa lugha ya Hopi aliyekuwa anaishi katika jiji la New York Marekani. Katika utafiti

huo alithibitisha kuwa wazungumzaji wa lugha ya Hopi hawazingatii sheria katika

upande wa nyakati (njeo) wanapozungumza, kwa hiyo ni lazima watu hao

wanausawiri wakati tofauti na watu wengine. Whorf (keshatajwa) alidai kuwa

wazungumzaji wa lugha fulani huzungumzia vitu fulani kwa urahisi kwa vile wana

Wataalamu hawa mwishoni waliungana na kuunda nadharia iliyojulikana kwa jina la

Nadharia ya Uumbaji ya Sapir- Whorf. Wataalamu hawa kwa pamoja wanadai kuwa,

muundo wa lugha huathiri jinsi ambavyo wazungumzaji wa lugha hiyo huufasiri

ulimwengu na kuathiri pia mielekeo ya maisha yao. Mawazo yao yaliungwa mkono na

Wardhaugh (1986) aliposema kuwa jamii fulani hutumia lugha kwa njia ambayo

inaashiria wanachoamini katika utamaduni wao. Kwa maelezo ya wataalamu hao ni

dhahiri kuwa, jamii fulani hutumia majina ambayo yanaashiria na kuakisi utamaduni

wa watu hao.

Sapir na Whorf wanaendelea kusema kuwa, kuna uhusiano uliopo baina ya lugha na

mawazo yaeleayo akilini mwa watu wa jamii moja itumiayo lugha. Lugha ina jukumu

na jukumu hilo sio tu kama njia ya kutolea mawazo, bali kama kifaa cha kujengea

wazo katika mawasiliano yetu. Lugha ndio msingi wa kuelewa ulimwengu wa jamii

husika. Lugha za jamii yakiwepo majina yanasaidia kufahamu utamaduni, historia,

mazingira, hali za kiuchumi na kisiasa katika jamii husika. Nadharia hii pia inasisitiza

kuwa lugha hufungamana na jamii na bila jamii hakuna lugha. Kwa vile majina ya

watu ni kipengele cha lugha ni dhahiri kuwa majina ya asili nayo yana uhusiano na

jamii husika. Nadharia hii ya Uumbaji imejengwa katika mihimili/ misingi ifuatayo:

(i) Lugha ndio msingi wa kuuelewa ulimwengu. Unapojifunza lugha ni kama

unatawaliwa na lugha hiyo. Hata dunia utakayoiumba akilini mwako itatokana

na dunia kama ilivyoratibiwa na wasemaji wake.

(ii) Fikra za mtu yeyote huamuliwa na lugha anayozungumza. Hii inamaanisha

kuwa, watu wanaufasili ulimwengu kulingana na jinsi unavyoendelezwa na

(iii) Lugha huathiri namna watu wanavyoumba ulimwengu wao. Hivyo, watu

wanaozungumza lugha fulani huuona na kuufasili ulimwengu tofauti na

wanaozungumza lugha nyingine.

(iv) Hakuna jamiilugha mbili zinazoweza kuwa sawa, hivyo, hata maana ya majina

katika jamii mbalimbali haziwezi kuwa sawa. Nadharia inasisistiza kuwa kama

wazungumzaji wa jamiilugha fulani hawatakuwa tayari kudumisha lugha yao ya

asili iliyobeba amali za jamii, kuna kila dalili kwamba utambulisho wa

jamiilugha inaweza kupotea.

Ikiwa tabia za watu huathiriwa na lugha yakiwemo majina, basi ni vigumu

wanaotumia majina ya lugha nyingine kuelewana na kuafikiana maishani. Ikiwa

tutafuata usemi huu, basi ni wazi kwamba lugha zetu za kwanza yakiwepo majina

ambayo tunatumia kufikiria ndiyo yaliyo na nguvu juu ya fikra, matendo na

utamaduni wetu. Tunapotumia majina mengine basi hatuna budi kuyapa kipaumbele

majina ya asili ambayo huumba fikra zetu.

Kwa kuwa hii ni nadharia na nadharia ni mwelekeo wa imani, wapo pia wanaopinga

nadharia hii ya Uumbaji ya Sapir-Whorf na wanatoa sababu zifuatazo:

(i) Nadharia ya Sapir-Whorf inafanya watu kuwa watumwa wa lugha zao ambazo

zinadaiwa kudhibiti fikra zao

(ii) Wanaanthropolojia wa utamaduni wamekubaliana kuwa watu wana uwezo wa

kitu kinachozungumzwa hata ingawa msamiati unaotumiwa ni tofauti. Kwa

mfano Wamarekani wana msamiati mwingi wa magari, lakini haimaanishi watu

(iii) Kama tungekuwa watumwa wa lugha zetu yakiwepo majina basi watu wawili

wanaoishi nyumba moja na wanaotumia majina ya asili wangefikiri sawa.

Licha ya pingarnizi hizi, nadharia hii inafaa sana katika utafiti huu. Sapir (1958) anaserna kuwa, lugha huwa kizuizi cha kuleta maendeleo, hasa masharnbani, kwa vile watu wengi warnepuuza dhima ya lugha katika kuleta maendeleo. Anadai kuwa, kusipokuwepo na uelewano baina ya rnzungurnzaji na mpokeaji habari, hakuna maendeleo yanayoweza kupatikana. Maoni hayo yanaungwa mkono na Musau (1999) aliposerna kuwa, rnaturnizi ya lugha za kwanza yanaweza kuleta maendeleo mcngi ya uchurni katika jarnii zetu. Anaserna mtaalamu wa kilimo anahitaji kuwafunza wakulima njia bora ya kilimo kwa kutumia lugha yao ya kwanza wanayoifahamu vizuri.

Kutokana na majina haya ya asili tunaweza kusema kwamba jina linatunza historia ya

jamii kwa usahihi kuliko hata maandishi ya vitabu vya historia. Hii ni kutokana na

ukweli kwamba vitabu visipotunzwa huweza kupoteza historia ya jamii husika kwa

kupoteza ubora wa maandishi, kuchanika au kupotea. Lakini kama majina yataendelea

kurithishwa kutoka kizazi kimoja hadi kingine ni dhahiri jamii zitaendeleza kutunza

historia ya jamii husika kwa kupokea kutoka vizazi tangulizi. Hii inatudokeza

kwamba majina yasiyo ya jamii husika hayawezi kueleza historia ya jamii hiyo kwani

majina hayo ni urithi wa jamii nyingine ambayo kwayo hutambulishwa.